Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 8:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Basi, watu wakaenda kuleta matawi, wakajenga vibanda kila mutu kwenye dari na kwenye baraza ya nyumba yake, kwenye baraza za nyumba ya Mungu, kwenye uwanja wa kiwanja cha Mulango wa Maji na kiwanja cha Mulango wa Efuraimu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 8:16
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku moja, wakati wa magaribi, Daudi aliamuka toka katika kitanda, akaenda kwenye dari ya nyumba ya kifalme. Alipokuwa anatembea kule juu, alimwona mwanamuke mumoja akioga na mwanamuke yule alikuwa muzuri sana kwa umbo.


Yoasi mufalme wa Israeli alimuteka Amazia mufalme wa Yuda mwana wa Yoasi mwana wa Ahazia kule Beti-Semesi. Halafu akauendea Yerusalema na kuubomoa ukuta wake kutoka kwenye Mulango wa Efuraimu mpaka kwenye Mulango wa Pembeni, umbali wa karibu metre mia mbili.


Yosafati akasimama katikati ya kusanyiko la watu wa Yuda na Yerusalema mbele ya kiwanja kipya cha nyumba ya Yawe,


Alijenga mazabahu za kuabudia jeshi la mbinguni kwenye viwanja vya nyumba ya Yawe.


Kwenye Mulango wa Chemichemi walipanda ngazi kuelekea muji wa Daudi, wakapita nyumba ya kifalme ya Daudi, na kuelekea nyuma kwenye ukuta mpaka kwenye Mulango wa Maji, upande wa mashariki wa muji.


Na kutoka pale, tukapitia kwenye Mulango wa Efuraimu, Mulango wa Yesana, Mulango wa Samaki, Munara wa Hananeli, Munara wa Mia moja mpaka kwenye Mulango wa Kondoo. Tulimalizia maandamano yetu kwenye Mulango wa Walinzi.


akishirikiana na watumishi wa hekalu waliokaa Ofeli, wakajenga upya sehemu inayoelekeana na Mulango wa Maji, upande wa mashariki na munara murefu.


Kisha watu wote, kwa nia moja, wakakusanyika katika Yerusalema kwenye kiwanja kinachokuwa karibu na Mulango wa Maji. Wakamwambia Ezra, mwandishi, alete kitabu cha sheria ya Musa ambayo Yawe aliwapa watu wa Israeli.


Kisha Ezra akawasomea watu wote wanaume na wanawake na yeyote aliyeweza kuelewa Sheria ya Musa akiwa mbele ya Mulango wa Maji tangu asubui mpaka saa sita za muchana. Watu wote wakatega masikio yao na kusikiliza kwa uangalifu kitabu cha Sheria.


Nyumba za Yerusalema na nyumba za wafalme wa Yuda, ndizo nyumba zote ambazo juu ya paa zao watu walifukiza ubani kwa kutambikia makundi ya nyota, na kuitolea miungu mingine sadaka za divai, zote zitageuzwa kuwa chafu kama Tofeti.


Wakaldea wanaoushambulia muji huu wataingia na kuuteketeza kwa moto; watauteketeza pamoja na nyumba ambazo juu ya paa zake ubani ulifukiziwa kwa mungu Bali na sadaka za divai zilitolewa kwa miungu mingine, kwa kunichokoza.


“Unapojenga nyumba, jenga ukuta pembeni ya paa, kusudi usihukumiwe kama mutu akianguka kutoka huko, na kufa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ