Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 8:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Hivyo wakatangaza katika miji yao yote na kule Yerusalema, wakisema: “Mwende kwenye milima, mulete matawi ya mizeituni, mizeituni ya pori, mihadasi, mingazi na miti mingine kwa kujenga vibanda, kama vile ilivyoandikwa.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 8:15
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Njiwa yule akamurudilia Noa saa za magaribi akiwa na tawi bichi la muzeituni katika midomo yake. Kwa hiyo Noa akajua kwamba maji yalikuwa yamepunguka katika inchi.


Sikukuu zingine zangu mimi Yawe ambazo mutakuwa na mukutano mutakatifu zitafanyika katika wakati huu uliopangwa.


Katika siku ya kwanza mutatwaa matunda ya miti yenu mizuri, matawi ya ngazi, matawi yenye majani mengi na matawi ya miti inayoota kandokando ya muto, nanyi mutafanya sikukuu mbele ya Yawe, Mungu wenu kwa siku saba.


Wakati wa usiku, nilimwona malaika akipanda juu ya farasi mwekundu. Malaika yule alikuwa akisimama katika bonde, katikati ya miti ya mihadasi. Nyuma yake kulikuwa farasi wengine wekundu, wa kijivujivu na weupe.


Yesu na wanafunzi wake wakakaribia kufika Yerusalema upande wa kijiji cha Betefage, karibu na mulima wa Mizeituni. Yesu akawatuma wawili kati ya wanafunzi wake,


Basi wakatwaa matawi ya ngazi na kwenda kumupokea, wakilalamika kwa sauti kubwa, wakisema: “Mungu asifiwe! Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Bwana! Abarikiwe mufalme wa Waisraeli!”


“Wanaume wote wa taifa lenu watakuja mbele ya Yawe, Mungu wenu, mara tatu kila mwaka, pahali ambapo Yawe, Mungu wenu atachagua: wakati wa sikukuu ya Pasaka, sikukuu ya kuvuna na wakati wa sikukuu ya vibanda. Wasitokee mbele ya Yawe mikono mitupu.


Kisha mambo haya, nikaangalia nami nikaona mukutano mukubwa sana wa watu wasioweza kuhesabiwa. Kulikuwa watu wa kila taifa, wa kila kabila, wa kila jamaa na wa kila luga. Walikuwa wakisimama mbele ya kiti cha kifalme na mbele ya Mwana-Kondoo, wakivaa kanzu nyeupe na kushika matawi ya muti wa ngazi katika mikono yao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ