vilevile alitoa maagizo juu ya kiasi cha zahabu safi iliyohitajika kwa kutengeneza makanya, mabeseni na vikombe, vilevile kiasi cha zahabu na feza iliyohitajika kwa kutengeneza mabakuli ya zahabu na ya feza,
Wakubwa wamoja wa ukoo walichangia kazi ya ujenzi. Mutawala wa jimbo alitoa kilo nane za zahabu, mabeseni makumi tano, nguo mia tano na makumi tatu ya makuhani.
Matoleo ya watu wengine wote yalikuwa kilo mia moja makumi sita na nane za zahabu, kilo mia moja makumi ine za feza na nguo za makuhani makumi sita na saba.
Watu waliposikia Sheria, wakaguswa ndani ya mioyo yao, halafu wote wakaanza kulia. Hivyo Nehemia aliyekuwa mutawala na Ezra kuhani na mwandishi, pamoja na Walawi waliofundisha watu wakawaambia watu wote: “Siku hii ni siku takatifu kwa Yawe, Mungu wenu, hivyo musiomboleze wala kulia.
Mutatwaa majani ya hisopo na kuyachovya katika damu ndani ya beseni na kupakaa vizingiti na miimo yote miwili ya milango ya nyumba zenu. Mutu yeyote asitoke inje ya nyumba usiku ule mpaka asubui.
Yule mukubwa wa waaskari walinzi wa mufalme alipeleka vibakuli, vyetezo, mabeseni, vyungu, vinara vya taa, vijiko vikubwa na mabakuli ya sadaka za vinywaji, vyombo hivyo vikiwa vya zahabu au vya feza.