61 Watu walirudi kutoka miji hii: Teli-Mela, Teli-Harsa, Kerubu, Adoni, Imeri. Lakini haikuwezekana kuhakikisha kwamba walikuwa wazao wa Waisraeli.
Watu walirudi kutoka miji hii: Teli-Mela, Teli-Harsa, Kerubu, Adani na Imeri. Lakini hawakuweza kuhakikisha kwamba walikuwa wazao wa Waisraeli.
Watumishi wote wa hekalu na wazao wa watumishi wa Solomono, waliorudi kutoka katika uhamisho, walikuwa mia tatu makumi tisa na wawili.
Wao walikuwa wazao wa Delaya, Tobia na wa Nekoda, kwa jumla: watu mia sita makumi ine na wawili.