Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 6:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Na barua yenyewe iliandikwa hivi: Kuna habari zilizoenezwa kati ya mataifa jirani, na Gesemi anahakikisha habari hizi, kwamba wewe pamoja na Wayuda wenzako munakusudia kuasi. Hii ndiyo sababu munaujenga upya ukuta. Kulingana na habari hizo, wewe unakusudia kuwa mufalme wao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 6:6
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tungependa ufahamu, ewe mufalme, kwamba Wayuda waliokuja hapa kutoka maeneo mengine ya ufalme wako wamekwenda Yerusalema na wanaujenga upya muji huo wa waasi na waovu. Wanamalizia kujenga kuta zake na kutengeneza musingi.


kusudi ufanye uchunguzi katika kitabu cha habari za babu zako. Humo utagundua kwamba tangu zamani, muji huu ulikuwa wa waasi na umewasumbua sana wafalme na watawala wa majimbo, na kuwa tangu zamani watu wake ni wachochezi sana; ndiyo sababu muji huo uliangamizwa.


Lakini Sanibalati, Muhori, Tobia, Mwamoni mutumishi wake, na Gesemi, Mwarabu, waliposikia hayo, wakatucheka na kutuzomea wakisema: “Ni kitu gani hiki munachotenda? Munataka kumwasi mufalme?”


Alikuwa amelipwa kwa kunitisha kusudi nifanye zambi. Na kwa njia hii wangepata njia ya kuchafua jina langu kwa kunishushia heshima yangu.


Kwa mara ya tano, Sanibalati akanitumia barua yenye kuwa wazi kwa njia ya mujumbe wake.


Kwa kuhakikisha wazo lako, umejiwekea manabii katika Yerusalema kusudi watangaze kwamba kuna mufalme katika inchi ya Yuda. Maneno haya yataelezwa kwa mufalme Artasasta. Hivyo ninashauri kwamba wewe na mimi tukutane na kuzungumuzia jambo hili.


Ninasikia watu wengi wakinisingizia uongo, nao wananipanga jina la Kitisho Kila Pahali! Wengine wanasema: Tumushitaki, Tumushitaki! Rafiki zangu wapenzi wote wanangojea kwa hamu nianguke! Wanasema: Labda atadanganyika, tupate kumunasa na kumulipiza kisasi.


“Heri ninyi, wakati watu wanapowatukana na kuwatesa na kuwasingizia kila namna ya ubaya kwa sababu yangu.


Wakaanza kumushitaki, wakisema: “Tulimukuta mutu huyu akiwashawishi watu wa taifa letu kufanya uasi. Yeye alikuwa akiwaambia kwamba wasilipe kodi kwa Mufalme wa Roma. Na zaidi ya hii anasema kwamba yeye ndiye Kristo, Mufalme aliyengojewa.”


Pilato aliposikia maneno haya, akamupeleka Yesu inje; akaikaa katika kiti cha hukumu kwenye nafasi inayoitwa katika Kiebrania “Gabata,” maana yake “Sakafu ya Mawe.”


Ikiwa ni vile, basi tuseme: “Tufanye mabaya kusudi kutokee mema”? Hakika kuna watu wamoja wanaonisingizia wakisema kwamba nimesema vile. Watu hawa wataazibiwa sawa inavyowapasa!


Tunaheshimiwa na kuzarauliwa, tunatukanwa na kusifiwa. Tunahesabiwa kama wenye kusema uongo, ingawa sisi tunasema ukweli,


mukiwa na zamiri safi, hata wale wanaowasingizia na kuwatukana juu ya mwenendo wenu muzuri katika ushirika wenu na Kristo, wapate haya.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ