Wengi kati ya Wayuda walishirikiana naye kutokana na kiapo chao maana alikuwa mukwe wa Sekania mwana wa Ara. Zaidi ya yote, Yehohanani mwana wake, alikuwa amemwoa binti Mesulamu mwana wa Berekia.
Walifanya hivyo kwa kututisha wakifikiri: “Hawataendelea na kazi, kwa hiyo, hakuna litakalotendeka.” Nikamwomba Mungu wangu nikisema: “Lakini sasa, ee Mungu, ninakuomba unipe nguvu.”
Kama mungekuwa watu wa dunia, dunia ingewapenda, kwa maana ninyi ni watu wake. Lakini nimewachagua ninyi toka dunia hii, na ninyi si watu wa dunia tena. Ni kwa sababu hii dunia inawachukia.