Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 6:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Lakini mimi nikajiuliza ndani ya moyo: “Mutu kama mimi ataweza kukimbia? Mutu kama mimi anahitaji kuingia katika hekalu apate kuponyesha maisha yake? Sitaingia hata kidogo katika hekalu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 6:11
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nikatambua kwamba hakutumwa na Mungu, lakini alikuwa amelipwa na Tobia na Sanibalati atangaze mabaya juu yangu.


Basi, nikawatumia wajumbe, nikisema: “Kazi ninayoifanya ni ya lazima sana. Hivyo siwezi kufika kwenu kusudi kazi isipate kusimama.”


Walifanya hivyo kwa kututisha wakifikiri: “Hawataendelea na kazi, kwa hiyo, hakuna litakalotendeka.” Nikamwomba Mungu wangu nikisema: “Lakini sasa, ee Mungu, ninakuomba unipe nguvu.”


Hatashindwa hata kidogo; atakumbukwa milele.


Yuko imara ndani ya moyo, wala hataogopa; naye ataona waadui zake wakishindwa.


Waovu wanakimbia ijapokuwa hawafukuzwi na mutu, lakini wenye haki ni hodari kama simba.


Mainzi waliokufa wanaharibu na kunukisha marasi; upumbafu kidogo unapoteza hekima na heshima.


Pori yake yenye utukufu na mashamba yake mazuri, Yawe atayaangamiza yote; itakuwa kama mutu aliyemalizika na ugonjwa.


Utachagua Haruni na wana wake kusudi waweze kutimiza kazi zao za ukuhani; lakini kama mutu yeyote mwingine akikaribia, atauawa.


Lakini sihesabu maisha yangu kuwa kitu cha bei kali kwangu. Shabaha moja ninayokuwa nayo ni kufikia mwisho wa utumishi wangu na kutimiza kazi ile niliyopewa na Bwana Yesu; maana yake kushuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.


Lakini Paulo akajibu: “Kwa sababu gani munalia na kunivunja moyo? Mimi niko tayari, si kwa kufungwa tu kule Yerusalema, lakini hata kufa vilevile kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.”


Naye Saulo alikuwa amekubali kwamba Stefano anastahili kuuawa. Siku ile ile kanisa lililokuwa katika Yerusalema lilianza kupata mateso makubwa. Waamini wote walisambaa katika Yudea na Samaria, isipokuwa mitume tu.


Hata nikitoa maisha yangu kuwa sadaka pamoja na imani yenu inayokuwa sadaka mbele ya Mungu, mimi ninafurahi na kushiriki pamoja nanyi wote.


kwa sababu yeye alikuwa karibu kufa kwa ajili ya kazi ya Kristo. Alihatarisha maisha yake kwa kuja kuniletea musaada ule ambao ninyi wenyewe musingeweza kunipatia.


Kwa njia ya imani, Musa alitoka katika inchi ya Misri bila kuogopa kasirani ya mufalme. Na kama vile mutu mwenye kumwona Mungu asiyeonekana, yeye hakurudi nyuma.


Alipomwua yule Mufilistini Goliati, alihatarisha maisha yake, naye Yawe aliwapa Waisraeli ushindi mukubwa. Wewe ulipoona jambo lile ulifurahi. Kwa nini unataka kutenda zambi kwa kumwanga damu isiyokuwa na kosa kwa kumwua Daudi bila sababu?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ