Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 6:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Nilipokwenda kwa Semaya mwana wa Delaya mujukuu wa Mehetabeli, ambaye hakuruhusiwa kutoka kwake, akaniambia: “Twende tukutane katika nyumba ya Mungu na milango yake tuifunge kwa sababu leo usiku watakuja kukuua.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 6:10
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Bali-Hanani mwana wa Akibori alipokufa, Hadari akatawala pahali pake, na jina la muji wake likiwa Pau. Muke wa Akibori alikuwa Mehetabeli, binti ya Matiredi, binti ya Mezahaba.


Tena aliongeza kujenga nguzo kuzunguka, kwa kutegemeza ukuta wa inje. Akatengeneza vyumba vya pembeni kila upande.


Yoasi alikaa naye kwa muda wa miaka sita akiwa amefichwa ndani ya nyumba ya Yawe, wakati Atalia alipokuwa akitawala katika inchi.


Utafanya hivyo kwa sababu jamaa yote ya Ahabu itaangamia. Tena nitamwua kila mwanaume wa jamaa ya Ahabu akuwe mutumwa au mutu huru.


Zaidi ya hayo, alikusanya vifaa vyote vya nyumba ya Mungu, akavikatakata vipandevipande, kisha akafunga milango ya nyumba ya Yawe na kujijengea mazabahu katika kila pembe ya Yerusalema.


Katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa kwanza wa utawala wake, mufalme Hezekia akafungua tena milango ya hekalu, akaitengeneza.


Tena, wamefunga milango ya baraza, wakazimisha taa, na hawajafukiza ubani wala kutoa sadaka za kuteketeza kwa moto katika Pahali Patakatifu pa Mungu wa Israeli.


Wazao wa Harimu: Eliezeri, Isia, Malkia, Semaya, Simeoni,


Nikaita viongozi tisa wakuje kwangu: Eliezeri, Arieli, Semaya, Elnatani, Yaribu, Elnatani, Natani, Zekaria na Mesulamu, pamoja na waalimu wawili, Yoyaribu na Elnatani.


Nikatambua kwamba hakutumwa na Mungu, lakini alikuwa amelipwa na Tobia na Sanibalati atangaze mabaya juu yangu.


Unisaidie, ee Yawe! Watu wema wamekwisha; waaminifu wametoweka kati ya watu.


Mwovu anamufanyia mutu wa haki shauri baya, na kumusagia meno kwa chuki.


Asiyemwogopa Mungu anaangamiza wengine kwa kinywa chake, lakini mwenye haki anaokolewa kwa maarifa yake.


Kisha, Yeremia akamupa Baruku maagizo haya: Mimi siruhusiwi kwenda katika nyumba ya Yawe.


Lakini roho ya Mungu aliniingia na kunisimamisha wima. Kisha Mungu akaongea nami, akaniambia: Kwenda ujifungie ndani ya nyumba yako.


Heri kungepatikana mutu mumoja kati yenu ambaye angefunga milango ya hekalu kusudi musiwashe moto usiokubaliwa kwenye mazabahu yangu! Sipendezwi nanyi na sitaikubali sadaka yoyote munayonitolea.


“Mufanye angalisho na manabii wa uongo; kwa maana wanakuja kwenu wakionekana kwa inje kama vile kondoo, lakini ndani, wao ni kama imbwa wakali wa pori.


Kila mutu anayefanya mabaya anachukia mwangaza, naye anakataa kuja kwenye mwangaza, kusudi matendo yake yasionekane wazi.


Muji wote ukajaa fujo na watu wakakusanyika pale mbiombio. Wakamukamata Paulo na kumukokotea mpaka inje ya hekalu, na mara moja wakafunga milango yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ