Ikiwa watu hao wanaleta biashara au ngano kwa kuuzisha siku ya Sabato, sisi hatutanunua siku hiyo wala siku nyingine yoyote inayokuwa takatifu. Mwaka wa saba hatutalima mashamba na madeni yote tutayafuta.
Leo hii muwarudishie mashamba yao, mashamba yao ya mizabibu, mashamba ya mizeituni na nyumba zao, hata na faida ya feza, ngano, divai, na mafuta ambayo mulikuwa munawalipisha.”
Mafungo ninayotaka mimi ni haya: kuwafungua waliofungwa bila haki, kuziondoa kamba za utumwa, kuwaacha huru wanaogandamizwa, na kuvunja kabisa mambo yote ya kitumwa!
Basi, kwa sababu tunajua kwamba ni lazima kumwogopa Bwana, ndiyo maana tunajitoa kuwavuta watu kwake. Mungu anatujua waziwazi nami ninatumaini kwamba ninyi wenyewe munatujua waziwazi vilevile.
Basi sisi ni wajumbe wa Kristo. Kwa njia yetu, Mungu mwenyewe anawaita ninyi; na kwa hiyo tunawasihi katika jina la Kristo, mukubali kupatanishwa na Mungu.
Hivi ndivyo mutakavyofanya: kila mumoja aliyemukopesha mwenzake, afute lile deni, wala asijaribu kumudai kwa sababu Yawe mwenyewe ameamua deni hilo lifutwe.