Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 4:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Ukiwa pahali popote unapofanya kazi, mara utakaposikia baragumu, kimbilia kwetu. Mungu wetu atatupigania.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 4:14
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini ujipe moyo! Tupigane kama wanaume kwa ajili ya watu wetu na kwa ajili ya miji ya Mungu wetu. Naye Yawe atutendee lile analoona ni jema kwake.”


“Muwe imara na hodari. Musiogope wala musifazaike mbele ya mufalme wa Asuria au majeshi yake maana tunayekuwa naye ni mukubwa kuliko anayekuwa na Saniharibu.


nikisema: “Ee Yawe, Mungu wa mbinguni, wewe ni Mungu unayekuwa mukubwa na wa kutisha, unashika agano lako na kutenda mema kwa wale wanaokupenda na kushika amri zako.


Mwangaza muzuri unatokea upande wa kaskazini; Mungu amezungukwa na utukufu wa kutisha.


Ninakumbuka siku za zamani, ninafikiri juu ya yote uliyotenda, ninawazawaza matendo yako.


Ninajua Yawe atamusaidia mufalme aliyemuchagua, atamujibu tokea pahali pake patakatifu mbinguni; kwa mukono wake wenye nguvu atamujalia ushindi mukubwa.


Zaburi ya Daudi. Yawe ni mwangaza wangu na wokovu wangu, ni nani nitakayemwogopa? Yawe ni mulinzi wa maisha yangu, sitamwogopa mutu yeyote.


Anasema: “Munyamaze na kujua kwamba mimi ni Mungu! Mimi ninatukuzwa katika mataifa yote; mimi ninatukuzwa katika ulimwengu wote!”


Heri wale unaowachagua na kuwaleta karibu, waishi katika kiwanja chako. Sisi tutatoshelewa na mazuri ya nyumba yako, mazuri ya hekalu lako takatifu.


Mumwambie Mungu: “Matendo yako ni ya ajabu! Kwa nguvu yako kubwa waadui zako wanaishiwa nguvu.


Mukuje muone mambo Mungu aliyotenda; ametenda mambo ya kutisha kati ya watu.


Yawe atawapigania. Ninyi mutakaa kimya tu.”


Alikwamisha magurudumu ya magari yao, yakakuwa yakienda kwa shida sana. Halafu Wamisri wakasema: “Tuwakimbie Waisraeli! Yawe anawapigania Waisraeli mbele yetu.”


Ukumbuke Muumba wako siku za ujana wako wakati hazijafika siku mbaya wala haijakaribia miaka utakaposema: “Sina furaha katika vitu hivyo.”


Atawashawishi kwa werevu wale walioasi agano, lakini watu wanaokuwa waaminifu kwa Mungu wao watasimama imara na kutenda.


Kisha Yawe atatoka na kuyapiga vita mataifa hayo, kama vile anavyofanya siku zote wakati wa vita.


Lakini musimwasi tu Yawe, wala musiwaogope wenyeji wa inchi hiyo. Maana wao ni kama mboga tu kwetu. Kingo yao imekwisha kuondolewa kwao naye Yawe yuko pamoja nasi. Musiwaogope!


Musiwaogope wale wanaoweza kuua tu mwili, lakini wasioweza kuua roho. Lakini zaidi mumwogope Mungu anayeweza kuharibu mwili pamoja na roho katika jehenamu.


Muangalie, Yawe, Mungu wenu, ameiweka inchi hii mbele yenu. Basi! Muende, muirizi kama vile Yawe, Mungu wa wazee wenu alivyowaambia. Musiogope wala musifazaike!’


Maana Yawe, Mungu wenu, ndiye Mungu wa miungu na Bwana wa wabwana. Yeye ni Mungu mukubwa na mwenye nguvu, na wa kuogopesha. Hapendelei wala hapokei kituliro.


Kwa sababu hii tunaweza kusema kwa uhodari: “Bwana ndiye musaidizi wangu; sitaogopa kitu. Mwanadamu ataweza kunifanya nini?”


Kumbuka kwamba mimi nimekuamuru ukuwe imara na hodari. Usiogope wala usifazaike kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, niko pamoja nawe popote utakapoenda.”


Alipofika kule akapiga baragumu katika inchi ya milima ya Efuraimu, nao Waisraeli wakateremuka pamoja naye kutoka kule kwenye milima naye akawatangulia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ