Na kutoka pale, tukapitia kwenye Mulango wa Efuraimu, Mulango wa Yesana, Mulango wa Samaki, Munara wa Hananeli, Munara wa Mia moja mpaka kwenye Mulango wa Kondoo. Tulimalizia maandamano yetu kwenye Mulango wa Walinzi.
Basi Eliasubu, Kuhani Mukubwa, pamoja na wandugu zake waliokuwa makuhani wakasimama na kuanza kujenga Mulango wa kondoo. Wakautakasa na kutia milango yake; wakaitakasa tangia kwenye Munara wa Mia Moja mpaka Munara wa Hananeli.
Sehemu inayofuata, tokea kwenye nyumba ya watumishi wa hekalu na wachuuzi iliyokuwa inaelekeana na Mulango wa Gereza, karibu na chumba cha juu kwenye pembe upande wa kaskazini-mashariki ikajengwa upya na Malkiya, mufua zahabu.
Sehemu inayofuata, ilijengwa upya na Usieli mwana wa Harihaya, mufua zahabu. Sehemu inayofuata mpaka kwenye Ukuta Mupana ikajengwa upya na Hanania, mutengenezaji wa marasi.
Kule Yerusalema, karibu na mulango wa muji huu unaoitwa “Mulango wa Kondoo,” kuna kisima chenye viingilio vitano vyenye paa. Kisima kile kinaitwa katika Kiebrania “Betesaida.”