Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 3:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 akishirikiana na watumishi wa hekalu waliokaa Ofeli, wakajenga upya sehemu inayoelekeana na Mulango wa Maji, upande wa mashariki na munara murefu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 3:26
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wa kwanza kurudia katika miji ya inchi yao walikuwa Waisraeli wa kawaida, makuhani, Walawi na watumishi wa hekalu.


Yotamu alijenga mulango wa kaskazini wa nyumba ya Yawe na kushugulika sana na ujenzi wa ukuta sehemu ya Ofeli.


Nyuma ya hayo, Manase akajenga ukuta mwingine upande wa inje wa muji wa Daudi, upande wa magaribi wa Gihoni, katika bonde, akauendelesha mpaka kwenye Mulango wa Samaki, akauzungusha Ofeli; akauinua juu sana. Pamoja na hayo, akaweka majemadari wa majeshi katika miji yote ya inchi ya Yuda yenye kuta.


Lakini watumishi wa hekalu walikaa Yerusalema katika eneo la Ofeli wakiwa chini ya usimamizi wa Ziha na Gisipa.


Kwenye Mulango wa Chemichemi walipanda ngazi kuelekea muji wa Daudi, wakapita nyumba ya kifalme ya Daudi, na kuelekea nyuma kwenye ukuta mpaka kwenye Mulango wa Maji, upande wa mashariki wa muji.


Sehemu ingine inayofuata, ikitokea kwenye munara murefu mpaka kwenye ukuta wa Ofeli ikajengwa upya na wakaaji wa muji wa Tekoa.


Kisha watu wote, kwa nia moja, wakakusanyika katika Yerusalema kwenye kiwanja kinachokuwa karibu na Mulango wa Maji. Wakamwambia Ezra, mwandishi, alete kitabu cha sheria ya Musa ambayo Yawe aliwapa watu wa Israeli.


Basi, watu wakaenda kuleta matawi, wakajenga vibanda kila mutu kwenye dari na kwenye baraza ya nyumba yake, kwenye baraza za nyumba ya Mungu, kwenye uwanja wa kiwanja cha Mulango wa Maji na kiwanja cha Mulango wa Efuraimu.


Kisha Ezra akawasomea watu wote wanaume na wanawake na yeyote aliyeweza kuelewa Sheria ya Musa akiwa mbele ya Mulango wa Maji tangu asubui mpaka saa sita za muchana. Watu wote wakatega masikio yao na kusikiliza kwa uangalifu kitabu cha Sheria.


Maana nyumba ya kifalme itaachwa ukiwa, muji huo wa watu wengi utahamwa. Mulima na munara wa ulinzi utakuwa mapango milele, punda wa mwitu watapitapita huko kwa furaha, kondoo watapata malisho yao humo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ