Mumoja kati ya wana wa Yoyada mwana wa Kuhani Mukubwa Eliasibu, alioa binti wa Sanibalati kutoka muji wa Beti-Horoni, kwa sababu hiyo nikamufukuza kutoka mbele yangu.
Basi Eliasubu, Kuhani Mukubwa, pamoja na wandugu zake waliokuwa makuhani wakasimama na kuanza kujenga Mulango wa kondoo. Wakautakasa na kutia milango yake; wakaitakasa tangia kwenye Munara wa Mia Moja mpaka Munara wa Hananeli.
Sehemu inayofuata tangia kwenye mulango wa nyumba ya Eliasibu, Kuhani Mukubwa, mpaka mwisho wa nyumba hiyo, ikajengwa upya na Meremoti mwana wa Uria, mujukuu wa Hakosi.