Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 3:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Sehemu inayofuata mpaka kwenye makaburi ya Daudi, kisima na majengo ya waaskari ikajengwa upya na Nehemia mwana wa Aibuki, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Beti-Suri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 3:16
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Matendo mengine ya Hezekia, ushujaa wake na maelezo juu ya jinsi alivyojenga kisima na kuchimba mufereji wa kuleta maji katika muji, yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.


Akazikwa katika kaburi alilokuwa amejichimbia yeye mwenyewe, katika muji wa Daudi. Walimulalisha juu ya kitanda kilichokuwa kimejazwa marasi ya kila aina yaliyotayarishwa na wafundi wa kutengeneza marasi, wakawasha moto mukubwa sana kwa heshima yake.


Halafu, nikaenda kwenye Mulango wa Chemichemi na kwenye Ziwa la Mufalme. Lakini yule punda niliyepanda juu yake hakuweza kupita.


Sehemu inayofuata ikajengwa upya na Salumu mwana wa Halohesi, mutawala wa nusu nyingine ya wilaya ya Yerusalema. Alisaidiana na binti zake katika ujenzi huo.


Mulango wa Yalala ukajengwa upya na Malkiya mwana wa Rekabu, mukubwa wa wilaya ya Beti-Hakeremu. Akaweka mulango kwa nafasi yake, akatia vyuma na vifungio vyake.


Nyuma ya hao, Walawi waliendelesha ujenzi mupya wa ukuta. Sehemu inayofuata ikajengwa upya na Rehumu mwana wa Bani, na Hasabia, mutawala wa nusu ya wilaya ya Keila, akajenga upya sehemu ya upande wa wilaya yake.


Sehemu inayofuata ikajengwa upya na Refaya mwana wa Huri, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Yerusalema.


Nilijichimbia visima vya maji ya kumwangilia ile miti.


Angalia! Ni kipoyi cha Solomono, akibebwa juu ya kiti chake cha kifalme, akizungukwa na walinzi makumi sita, mashujaa bora wa Israeli.


Katikati ya kuta hizo mulijijengea birika la kulinda maji yanapotiririka kutoka birika la zamani. Lakini hamukumutafuta Mungu aliyepanga mambo haya yote; hamukumujali yeye aliyepanga hayo yote tangu zamani.


mukaona kwamba nyufa za kuta za muji wa Daudi ni nyingi, mukajaza maji ndani ya birika la chini.


Yawe akamwambia Isaya: Uende pamoja na mwana wako anayeitwa Watakaobaki-Watarudi, kukutana na mufalme Ahazi. Utamukuta katika barabara pahali wafuaji wa nguo wanapofanyia kazi, mwisho wa mufereji unaoleta maji kutoka kwenye birika la juu.


“Wandugu, inanipasa kuwaambia kwa uhodari juu ya babu yetu mukubwa Daudi. Yeye alikufa na kuzikwa, nalo kaburi lake lingali hata leo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ