Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 3:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Mulango wa Chemichemi ukajengwa upya na Salumu mwana wa Koli-Hoze, mukubwa wa wilaya ya Misipa. Akaufunika, akauweka mulango kwa nafasi yake, akatia vyuma na vifungio vyake. Kwenye Kisima cha Sela akajenga ukuta unaokuwa karibu na bustani ya kifalme mpaka kwenye ngazi zinazoshuka toka muji wa mufalme Daudi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 3:15
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Daudi alikaa kwenye kikingio hicho. Akakiita: “Muji wa Daudi.” Daudi akaongeza muji, akianzia uwanja wa Milo kuelekea ndani.


Basi, sehemu ya ukuta wa muji ukabomolewa, naye mufalme pamoja na waaskari wote wakakimbia wakati wa usiku wakipitia katika bustani ya mufalme kwenye mulango katikati ya kuta mbili, wakaenda upande wa Araba, ingawa Wababeli walikuwa wameuzunguka muji.


Mufalme Hezekia ndiye aliyefunga maji ya chemichemi ya Gihoni, akayachimbia mufereji na kuyapitisha chini moja kwa moja mpaka upande wa magaribi wa muji wa Daudi. Hezekia alijaliwa katika kila jambo alilofanya,


Kwenye Mulango wa Chemichemi walipanda ngazi kuelekea muji wa Daudi, wakapita nyumba ya kifalme ya Daudi, na kuelekea nyuma kwenye ukuta mpaka kwenye Mulango wa Maji, upande wa mashariki wa muji.


Halafu, nikaenda kwenye Mulango wa Chemichemi na kwenye Ziwa la Mufalme. Lakini yule punda niliyepanda juu yake hakuweza kupita.


Kisha nikawaambia: “Bila shaka munaona magumu yetu kwamba muji wa Yerusalema ni mabomoko na milango yake imeteketezwa kwa moto. Basi, tujenge tena ukuta wa Yerusalema kusudi tusifezeheshwe zaidi.”


Sehemu inayofuata ikajengwa upya na Salumu mwana wa Halohesi, mutawala wa nusu nyingine ya wilaya ya Yerusalema. Alisaidiana na binti zake katika ujenzi huo.


Mulango wa Yalala ukajengwa upya na Malkiya mwana wa Rekabu, mukubwa wa wilaya ya Beti-Hakeremu. Akaweka mulango kwa nafasi yake, akatia vyuma na vifungio vyake.


Sehemu inayofuata inayoelekeana na gala ya silaha kwenye pembe ya ukuta ikajengwa upya na Ezeri mwana wa Yesua, mutawala wa Misipa.


Waliowafuata hao katika kazi hiyo ya kujenga upya walikuwa Melatia, Mugibeoni; Yadoni, Mumeronoti pamoja na watu wa muji wa Gibeoni na Misipa waliokuwa chini ya uongozi wa mutawala wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati.


Sehemu inayofuata ikajengwa upya na Refaya mwana wa Huri, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Yerusalema.


Nilijichimbia visima vya maji ya kumwangilia ile miti.


Kwa sababu watu hawa wameyakataa maji ya Siloa yanayotiririka polepole, wakatetemeka mbele ya mufalme Resini na mufalme Peka mwana wa Remalia,


Kisha Yeremia akaenda Misipa kwa Gedalia mwana wa Ahikamu, akakaa naye pamoja na wanainchi waliobaki katika inchi.


Vilevile munazani kwamba wale watu kumi na wanane waliokufa munara ulipowaangukia kule Siloamu, walikuwa wakosaji kuliko wakaaji wengine wote wa Yerusalema?


na kumwambia: “Kwenda unawe uso katika kisima cha Siloamu” (maana ya jina hili ni “Aliyetumwa”). Basi yule kipofu akaenda na kunawa uso, akarudi akiwa mwenye kuona.


Watu wote wa Israeli, kutokea Dani mpaka Beri-Seba, pamoja na watu wa inchi ya Gileadi, wakakusanyika kule Misipa, mbele ya Yawe.


Nao watu wa kabila la Benjamina, wakapata habari kwamba watu wale wengine wa Israeli walikuwa wamekusanyika kule Misipa. Basi Waisraeli wakamwuliza yule mwanaume Mulawi: “Utuelezee, uovu ule ulifanyika namna gani?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ