Nehemia 2:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20025 Halafu nikamwambia mufalme: “Ee mufalme, ikikupendeza na ikiwa nimepata kukubaliwa mbele yako, ninakuomba unitume katika inchi ya Yuda kusudi niende kuujenga upya muji ambamo muko makaburi ya babu zangu.” အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
“Ikikupendeza, ewe mufalme, na kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ukiona ni vizuri nami nikikupendeza, tafazali, toa tangazo la kuvunja mipango ambayo Hamani alikuwa ameamuru itimizwe. Mipango hiyo ni ile ya mwana wa Hamedata, wa uzao wa Agagi, aliyopanga kwa kuwaangamiza Wayuda wote katika majimbo yote.
Basi, ujue na kufahamu jambo hili: tangu wakati amri itakapotolewa ya kujengwa upya Yerusalema mpaka kuja kwa yule aliyepakwa mafuta, yule anayekuwa mukubwa, ni muda wa majuma saba. Kwa muda wa majuma makumi saba na mawili, Yerusalema utajengwa upya, wenye barabara kubwa na kuta, lakini wakati huo utakuwa wa taabu.