Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 2:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Lakini Sanibalati, Muhori, Tobia, Mwamoni mutumishi wake, na Gesemi, Mwarabu, waliposikia hayo, wakatucheka na kutuzomea wakisema: “Ni kitu gani hiki munachotenda? Munataka kumwasi mufalme?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 2:19
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mumoja kati ya wana wa Yoyada mwana wa Kuhani Mukubwa Eliasibu, alioa binti wa Sanibalati kutoka muji wa Beti-Horoni, kwa sababu hiyo nikamufukuza kutoka mbele yangu.


Lakini Sanibalati wa muji wa Muhori na Tobia, Mwamoni, mutumishi wake, waliposikia kwamba nimekuja kwa kushugulikia hali njema ya watu wa Israeli, hawakufurahia kabisa jambo hilo.


Lakini Sanibalati, Tobia, Waarabu, Waamoni na Waasidodi waliposikia kwamba ujenzi mupya wa ukuta wa Yerusalema ulikuwa unasonga mbele na kwamba nafasi zilizobomoka katika ukuta zimezibwa, wao walizidi kukasirika.


Na barua yenyewe iliandikwa hivi: Kuna habari zilizoenezwa kati ya mataifa jirani, na Gesemi anahakikisha habari hizi, kwamba wewe pamoja na Wayuda wenzako munakusudia kuasi. Hii ndiyo sababu munaujenga upya ukuta. Kulingana na habari hizo, wewe unakusudia kuwa mufalme wao.


Walifanya hivyo kwa kututisha wakifikiri: “Hawataendelea na kazi, kwa hiyo, hakuna litakalotendeka.” Nikamwomba Mungu wangu nikisema: “Lakini sasa, ee Mungu, ninakuomba unipe nguvu.”


Lakini sasa watu wananichekelea, tena watu wanaokuwa wadogo kuliko mimi; watu ambao niliwaona baba zao hawafai hata kuwahesabu kama imbwa wangu wakilinda kondoo.


Tumeshiba muda murefu mazarau ya watajiri, nayo masimango ya wenye kiburi.


Tunazarauliwa na mataifa jirani, jirani zetu wanatuchekelea na kutusimanga.


Umefanya huzuni ikuwe chakula chetu; umetukunywesha machozi kwa wingi.


Umetufanya jambo la mazarau kwa jirani zetu; waadui zetu wanatuchekelea.


Unazani kwamba maneno matupu ndiyo maarifa na nguvu katika vita? Ni nani unayemutegemea hata ukaniasi?


Kila mara ninaposema kitu, ninalalamika, ninapandisha sauti kwa kutangaza mateso na uharibifu. Kutangaza neno la Yawe kunaniletea kuzomewa na kuzarauliwa kila siku.


Kisha, Isimaeli aliwakamata wabinti wa mufalme mateka na watu wote waliobaki kule Misipa, watu ambao Nebuzaradani, mukubwa wa walinzi, alikuwa amewaweka chini ya ulinzi wa Gedalia mwana wa Ahikamu. Isimaeli mwana wa Netania, aliwakamata mateka hao, akaondoka, akaenda kwa Waamoni.


Halafu akasema: “Mutoke hapa. Binti huyu mudogo hakukufa, lakini analala tu.” Nao wakaanza kumuchekelea.


Nao wakaanza kumuchekelea. Halafu Yesu akawaondosha wote inje, akawakamata wazazi wa yule mutoto na wanafunzi wake watatu, akaingia katika chumba pahali mutoto alipokuwa.


Wakaanza kumushitaki, wakisema: “Tulimukuta mutu huyu akiwashawishi watu wa taifa letu kufanya uasi. Yeye alikuwa akiwaambia kwamba wasilipe kodi kwa Mufalme wa Roma. Na zaidi ya hii anasema kwamba yeye ndiye Kristo, Mufalme aliyengojewa.”


Tokea saa ile Pilato alitafuta njia ya kumufungua Yesu. Lakini Wayuda wakapiga kelele, wakisema: “Ukimufungua mutu huyu, wewe si rafiki wa Mufalme wa Roma. Kila mutu anayejifanya kuwa mufalme, anamupinga Mufalme wa Roma!”


Tumetambua kwamba mutu huyu ni wa hatari sana, ameanzisha fujo kati ya Wayuda wote katika dunia. Tena yeye ni mukubwa wa chama cha Wanazareti.


Wengine walichekelewa na kupigwa fimbo, na wengine walifungwa minyororo na kutupwa katika kifungo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ