Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 2:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Kisha nikawaambia: “Bila shaka munaona magumu yetu kwamba muji wa Yerusalema ni mabomoko na milango yake imeteketezwa kwa moto. Basi, tujenge tena ukuta wa Yerusalema kusudi tusifezeheshwe zaidi.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 2:17
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Haukutuacha tuishi katika utumwa ingawa tulikuwa watumwa. Uliwafanya wafalme wa Persia wakuwe wema kwetu na kuturuhusu tuishi na kuijenga nyumba yako iliyokuwa imebomoka, na ukatufanya tukae salama hapa Yuda na Yerusalema.


Wao wakaniambia: “Wayuda walioponyoka na kubaki katika jimbo lile, wako katika taabu nao wanazarauliwa. Ukuta wa Yerusalema umebomolewa na milango yake imeteketezwa.”


Nikatoka nikipitia kwenye Mulango wa Bonde katika njia inayoelekea kwenye Kisima cha Joka na mulango wa Yalala; nikachunguza kuta za muji wa Yerusalema ambazo zilikuwa zimebomolewa pamoja na milango yake ambayo ilikuwa imeteketezwa kwa moto.


Wakubwa hawakujua pahali nilipokuwa nimekwenda wala nimefanya nini. Tena nilikuwa sijawaambia Wayuda, makuhani, viongozi, wakubwa wala wale watu ambao wangefanya kazi ya kujenga upya muji.


Mulango wa Chemichemi ukajengwa upya na Salumu mwana wa Koli-Hoze, mukubwa wa wilaya ya Misipa. Akaufunika, akauweka mulango kwa nafasi yake, akatia vyuma na vifungio vyake. Kwenye Kisima cha Sela akajenga ukuta unaokuwa karibu na bustani ya kifalme mpaka kwenye ngazi zinazoshuka toka muji wa mufalme Daudi.


Watumishi wako wanapenda muji ule, ijapokuwa ni mabomoko sasa; wanauonea huruma, ingawa umeharibika kabisa.


Umeuzisha watu wako kwa bei ya chini; wala haukupata faida yoyote.


Umetupotezea heshima mbele ya jirani zetu, nao wanatuchekelea na kutuzarau.


Ee Bwana, uwalipize mataifa jirani mara saba kwa ajili ya matusi waliyokutukana.


Tunazarauliwa na mataifa jirani, jirani zetu wanatuchekelea na kutusimanga.


Nitawafanya kuwa kitu cha kuchukiza mbele ya falme zote za dunia. Watakuwa kitu cha zihaka, kitu cha kuzomewa, kuchekelewa na kulaaniwa kila fasi nitakapowasambaza.


Yawe ameharibu bila huruma makao yote ya wazao wa Yakobo. Kwa kasirani yake amevibomoa vikingio vya watu wa Yuda. Ametupa chini na kuchafua ufalme wao na watawala wake.


Ninahuzini sana kuona yale yaliyowapata wabinti wa muji wangu.


Tena, wewe Yerusalema nitakufanya kuwa ukiwa na kitu cha kuchekelewa kati ya mataifa yanayokuzunguka na mbele ya watu wote wanaopita karibu nawe.


Siku inakuja ambapo kuta za muji wenu zitajengwa upya. Siku hiyo mipaka ya inchi yenu itapanuliwa.


Lakini akawaambia: “Nitafanya mapatano nanyi kwa shurti hii moja: nitamwongoa kila mumoja wenu jicho lake la kuume. Hivyo nitawapatisha Waisraeli wote haya.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ