Nyuma ya mambo haya yote kutendeka, viongozi wakanifikia na kunipa habari hii: “Watu wa Israeli, makuhani na Walawi hawakujitenga na wakaaji wa inchi ambao wanatenda machukizo: Waamoni, Wamoabu na Wamisri, Wakanana, Wahiti, Waperizi, Wayebusi na Waamori.
alimuruhusu Tobia kutumia chumba kikubwa ambamo pale mbele walikuwa wakiweka sadaka za unga, ubani, vyombo, zaka za unga, divai, mafuta; vitu hivyo vyote Waisraeli walivyoagizwa kutoa kwa Walawi, waimbaji, walinzi wa milango, na matoleo kwa makuhani.
Waadui wamenyoosha mikono yao, wapate kukamata vitu vyake vyote vya bei kali. Kweli umeona watu wa mataifa wakiingia ndani ya hekalu, watu ambao Yawe aliwakataza kuingia kati kusanyiko lake.