Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 13:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Wakati uleule, nikawaona watu wa Yuda wakikamua zabibu katika vikamulio siku za Sabato. Tena wengine walikuwa wakiwabebesha punda wao ngano, divai, zabibu, tini na vitu vingine wakivipeleka Yerusalema. Nikawaonya kwamba hawana ruhusa ya kuuzisha katika siku hiyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 13:15
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, akawatumia manabii kwa kuwaonya kusudi wamurudilie Yawe, lakini wao hawakuwasikiliza.


Wabinti zetu hatutawaoesha kwa watu wa inchi hii na wala wana wetu hawataoa kwao.


Ikiwa watu hao wanaleta biashara au ngano kwa kuuzisha siku ya Sabato, sisi hatutanunua siku hiyo wala siku nyingine yoyote inayokuwa takatifu. Mwaka wa saba hatutalima mashamba na madeni yote tutayafuta.


Watu wengine toka muji wa Tiro walileta samaki na biashara nyingine Yerusalema na kuwauzishia watu wetu siku ya Sabato.


Nikawaonya na kuwaambia: “Hakuna maana kulala inje ya muji. Mukijaribu tena nitatumia nguvu.” Hivyo tangu wakati ule hawakurudi tena siku ya Sabato.


Ukawaonya kusudi warudilie Sheria yako, hata hivyo, kwa kiburi chao, wakaacha kutii amri zako. Wakaasi maagizo yako, ambayo kwa njia yake mutu akiyatii, ataishi. Wakakuwa wenye kiburi vilevile wakakuwa wagumu, na wakakataa kuwa watiifu.


Unamutazamia mbogo akuvunie mavuno yako, na kuleta ngano kwenye nafasi ya kupepetea?


“Enyi watu wangu, munisikilize, mimi Mungu, Mungu wenu! Ninataka kusema nanyi. Israeli, ninakuonya.


Kwa hiyo Waisraeli watashika Sabato katika vizazi vyao vyote kama vile kitambulisho cha agano la milele.


Siku sita mutafanya kazi, lakini siku ya saba mutapumzika, hata ikiwa ni wakati wa kulima au kuvuna.


Kwa siku sita mutafanya kazi zenu. Lakini siku ya saba ni Sabato, siku ya mapumziko ambayo ni takatifu kwa Yawe. Yeyote atakayefanya kazi siku hiyo lazima auawe.


Watu wanaovunja sheria wanasifu waovu, lakini wanaoshika sheria wanapingana nao.


Kama ukiacha kufanya kazi siku ya Sabato, ukiacha shuguli zako siku yangu hiyo takatifu, ukiifanya siku yangu kuwa ya furaha, ukiheshimu siku hiyo takatifu ya Yawe, ukiacha shuguli zako au kupiga domo,


Lakini ninyi munisikilize mimi. Muache kuingiza muzigo wowote kupitia kwenye milango ya muji huu siku ya Sabato, muihesabu kuwa takatifu na kutofanya kazi.


Lakini musiponisikiliza na mukiacha kuihesabu siku ya Sabato kama siku takatifu, musipoacha kubeba mizigo na kuingia nayo kupitia milango ya Yerusalema siku ya Sabato, basi nitawakisha moto katika milango yake, nao utateketeza nyumba zote nzuri za Yerusalema, wala hautazimika. –Ni ujumbe wa Yawe.


Yeremia akawaambia watu: Enyi Wayuda muliobaki, Yawe aliwaambia musiende Misri. Mujue wazi kwamba leo nimewaonya kwamba


Lakini Waisraeli waliniasi kule katika jangwa; hawakuyafuata masharti yangu, lakini walikataa maagizo yangu ambayo mutu akiyafuata ataishi. Sabato zangu walizikufuru siku zote, nami nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuwaangamiza kulekule katika jangwa.


Munajisemesha ndani ya mioyo yenu: Sikukuu ya mwandamo wa mwezi itakwisha wakati gani kusudi tuanze tena kuuzisha vyakula vyetu? Siku ya Sabato itakwisha wakati gani kusudi tupate kuuzisha ngano yetu? Tutapunguza vipimo, tutapandisha bei, tutadanganya watu kwa mizani zisizokuwa sawa.


Anasema hivi: Enyi watu wangu, nimewatendea nini? Nimewachokesha kwa kitu gani? Munijibu!


Petro akazidi kusema maneno mengine ya kuwaonya na kuwatia moyo, akisema: “Mujiokoe toka kati ya kizazi hiki kipotovu!”


Nimewaonya Wayuda wa mataifa mengine kwamba wanapaswa kumugeukia Mungu na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.


Mimi ninasema tena wazi, kila mutu anayekubali kutahiriwa sherti ashike Sheria yote.


Basi, kwa jina la Bwana ninawaonya hivi: musiishi tena kama watu wa mataifa mengine, wanaofuata mawazo yao ya bure


Lakini mukimusahau Yawe, Mungu wenu, na kufuata miungu mingine kwa kuitumikia na kuiabudu, ninawaonya vikali leo hii kwamba hakika mutaangamia.


Kuelekea maneno hayo, mutu yeyote asimukosee ndugu yake wala kumudanganya. Tumekwisha kuwaambia na kuwahakikishia mbele kwamba Bwana atawaazibu wale wanaofanya mambo kama hayo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ