“Ee Yawe, ninakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote na kutenda mazuri mbele yako.” Hezekia akalia kwa uchungu sana.
Tena zaidi ya vyote nilivyotoa kwa ajili ya nyumba takatifu, nina hazina yangu ya pekee ya zahabu na feza, na kwa sababu ninapenda nyumba ya Mungu wangu ninaitoa kwa nyumba ya Mungu wangu;
Wakamuzika katika muji wa Daudi, kwenye makaburi ya wafalme kwa kuonyesha heshima yao kwake kwa sababu alifanya mema katika Israeli na mbele ya Mungu na nyumba yake.
Tunawafahamisha tena kwamba inakatazwa kuwadai kodi ya mapato, malipo ya kuvuka mupaka na mengine makuhani, Walawi, waimbaji, walinzi wa mulango, wafanyakazi au watumishi wengine wa nyumba hii ya Mungu.
Nikaagiza Walawi kujitakasa na kwenda kulinda milango kwa kutakasa siku ya Sabato. Ee, Mungu wangu, unikumbuke hata na kwa hili vilevile unihurumie kutokana na rehema zako kubwa.
Nikaagiza matoleo ya kuni kufanyika katika wakati unaopaswa na malimbuko wakati wake. Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa ajili ya haya yote na unijalie mema.
akisema: Ee Yawe, ninakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote, na kutenda mazuri mbele yako. Hezekia akalia kwa uchungu sana.
Kwa maana Mungu ni mwenye haki. Yeye hatasahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili yake kwa namna mulivyowasaidia watu wake na munavyoendelea kuwasaidia.
Yule atakayeshinda atavalishwa nguo nyeupe, nami sitafuta jina lake kati ya majina yanayoandikwa katika kitabu cha uzima. Nami nitamutetea mbele ya Baba yangu na mbele ya wamalaika zake.