Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 12:39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

39 Na kutoka pale, tukapitia kwenye Mulango wa Efuraimu, Mulango wa Yesana, Mulango wa Samaki, Munara wa Hananeli, Munara wa Mia moja mpaka kwenye Mulango wa Kondoo. Tulimalizia maandamano yetu kwenye Mulango wa Walinzi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 12:39
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yoasi mufalme wa Israeli alimuteka Amazia mufalme wa Yuda mwana wa Yoasi mwana wa Ahazia kule Beti-Semesi. Halafu akauendea Yerusalema na kuubomoa ukuta wake kutoka kwenye Mulango wa Efuraimu mpaka kwenye Mulango wa Pembeni, umbali wa karibu metre mia mbili.


Hivyo, makundi yote mawili yaliyokuwa yanaimba nyimbo za shukrani yakasimama katika nyumba ya Mungu, pamoja nami na nusu ya viongozi;


Basi Eliasubu, Kuhani Mukubwa, pamoja na wandugu zake waliokuwa makuhani wakasimama na kuanza kujenga Mulango wa kondoo. Wakautakasa na kutia milango yake; wakaitakasa tangia kwenye Munara wa Mia Moja mpaka Munara wa Hananeli.


Sehemu inayofuata, tokea kwenye pembe ya ukuta na munara wa nyumba ya kifalme ya juu karibu na kiwanja cha walinzi ikajengwa upya na Palali mwana wa Uzayi. Pedaya mwana wa Parosi,


Nao watu wa ukoo wa Hasena wakajenga upya Mulango wa Samaki, wakatia miimo yake, milango, vyuma na vifungio vyake.


Mulango wa zamani; ukajengwa upya na Yoyada mwana wa Pasea, pamoja na Mesulamu mwana wa Besodia, wakatia miimo yake, milango, vyuma na vifungio vyake.


Basi, watu wakaenda kuleta matawi, wakajenga vibanda kila mutu kwenye dari na kwenye baraza ya nyumba yake, kwenye baraza za nyumba ya Mungu, kwenye uwanja wa kiwanja cha Mulango wa Maji na kiwanja cha Mulango wa Efuraimu.


Siku zinakuja ambapo muji huu wa Yerusalema utajengwa upya kwa ajili ya Yawe, kutokea kwenye munara wa Hananeli mpaka kwenye mulango wa Pembe.


Wakati huo, waaskari wa mufalme wa Babeli walikuwa wakizunguka Yerusalema kwa vita, naye nabii Yeremia alikuwa amefungwa katika baraza la walinzi uliokuwa ndani ya nyumba ya mufalme wa Yuda.


Siku hiyo, kutasikilika kilio kutoka Mulango wa Samaki, maombolezo kutoka Mutaa wa Pili, na mulio mukubwa kutoka katika milima. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Kule Yerusalema, karibu na mulango wa muji huu unaoitwa “Mulango wa Kondoo,” kuna kisima chenye viingilio vitano vyenye paa. Kisima kile kinaitwa katika Kiebrania “Betesaida.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ