Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 12:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Nikawakusanya viongozi wote wa Yuda kwenye ukuta na kutenga waimbaji katika makundi mawili makubwa yaliyoimba nyimbo za shukrani wakiwa katika maandamano. Kundi moja lilielekea upande wa kuume wa ukuta mpaka kwenye Mulango wa Takataka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 12:31
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Daudi akashauriana na majemadari wa makundi ya maelfu na makundi ya mamia, pamoja na viongozi wote.


Mufalme Daudi akakusanya kule Yerusalema wakubwa wote wa Waisraeli: wa makabila, majemadari na vikundi waliomutumikia mufalme, wakubwa wa maelfu na mamia, wasimamizi wa mali yote, ya ngombe wote wa mufalme na wana wake pamoja na wakubwa wa nyumba ya kifalme, mashujaa na waaskari wenye heshima.


Basi mufalme Solomono akawakusanya kule Yerusalema wazee na viongozi wote wa makabila wa ukoo za Waisraeli kusudi waondoe Sanduku la Agano la Yawe kutoka katika muji wa Daudi, ni kusema Sayuni.


Waimbaji hao walifuatwa na Hosaya akiwa pamoja na nusu ya viongozi wa Yuda.


Kundi lingine lililoimba nyimbo za shukrani lilielekea upande wa kushoto juu ya ukuta. Mimi nikafuatana na kundi hili pamoja na nusu ya watu. Tukapitia kwenye Munara wa Furu mpaka kwenye Ukuta Mupana.


Hivyo, makundi yote mawili yaliyokuwa yanaimba nyimbo za shukrani yakasimama katika nyumba ya Mungu, pamoja nami na nusu ya viongozi;


Nikatoka nikipitia kwenye Mulango wa Bonde katika njia inayoelekea kwenye Kisima cha Joka na mulango wa Yalala; nikachunguza kuta za muji wa Yerusalema ambazo zilikuwa zimebomolewa pamoja na milango yake ambayo ilikuwa imeteketezwa kwa moto.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ