Nehemia 12:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200227 Kisha wakati wa kuzindua ukuta wa Yerusalema Walawi wakatafutwa kila pahali walipokaa kwa kuja Yerusalema kusherehekea kwa furaha pamoja na shukrani na nyimbo, wakitumia matoazi, vinubi na zeze. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Hao ndio Walawi, wazao wa Haruni, ambao Daudi aliowaita kufuatana na ukoo zao: Ukoo wa Kohati: Urieli na wandugu zake mia moja na makumi mbili chini ya usimamizi wake; Ukoo wa Merari: Asaya na wandugu zake mia mbili na makumi mbili chini ya usimamizi wake; Ukoo wa Gersoni: Yoeli na wandugu zake mia moja na makumi tatu chini ya usimamizi wake; Ukoo ya Elisafani: Semaya na wandugu zake mia mbili chini ya usimamizi wake; Ukoo wa Hebroni: Elieli na wandugu zake makumi munane chini ya usimamizi wake; Ukoo wa Uzieli: Aminadabu na wandugu zake mia moja kumi na wawili, chini ya usimamizi wake.
Makuhani walikuwa wakisimama kwenye nafasi za kazi zao, nao Walawi, walisimama wakiwa na vyombo vya Yawe vya muziki mufalme Daudi alivyotengeneza kwa ajili ya kutoa shukrani kwa Yawe. Waliimba: “Wema wake unadumu milele.” Wakati Daudi alipotoa shukrani, walimusaidia; makuhani walipiga baragumu nao Waisraeli wote wakasimama.