Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 12:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Kisha wakati wa kuzindua ukuta wa Yerusalema Walawi wakatafutwa kila pahali walipokaa kwa kuja Yerusalema kusherehekea kwa furaha pamoja na shukrani na nyimbo, wakitumia matoazi, vinubi na zeze.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 12:27
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Daudi aliposikia kwamba Yawe ameibariki jamaa ya Obedi-Edomu na vitu vyote alivyokuwa navyo kwa sababu ya Sanduku la Mungu, akaenda kuliondoa Sanduku la Agano kutoka katika nyumba ya Obedi-Edomu na kulipeleka kwenye muji wa Daudi kwa shangwe.


Naye Solomono alimutolea Yawe sadaka za amani: ngombe elfu makumi mbili na mbili na kondoo elfu mia moja na makumi mbili. Hivi ndivyo mufalme na watu wote wa Israeli walivyozindua nyumba ya Yawe.


Daudi na Waisraeli wote wakakuwa wanacheza kwa nguvu zao zote, mbele ya Mungu. Waliimba nao wakikuwa wanapiga ala za muziki zilizotengenezwa kwa muti wa muvinje: vinubi, vinanda, matari, matoazi na baragumu.


akawaambia: “Ninyi ni viongozi wa ukoo za Walawi. Mujitakase pamoja na wandugu zenu, mupate kuleta Sanduku la Agano la Yawe, Mungu wa Israeli, mpaka pahali ambapo nimelitayarishia.


Daudi aliwaamuru vilevile wakubwa wa Walawi wachague kati ya wandugu zao waimbaji wakuwe wanaimba na kupiga ala za muziki kwa nguvu, kwa kutoa sauti za furaha. Walipiga vinanda, vinubi na matoazi.


Hivyo, Waisraeli wote wakakusanyika pamoja kwa shangwe kwa kubeba Sanduku la Agano la Yawe mpaka Yerusalema. Wakalisindikiza kwa mulio wa baragumu, ngunga, matoazi, na sauti kubwa za vinanda na vinubi.


Hao ndio Walawi, wazao wa Haruni, ambao Daudi aliowaita kufuatana na ukoo zao: Ukoo wa Kohati: Urieli na wandugu zake mia moja na makumi mbili chini ya usimamizi wake; Ukoo wa Merari: Asaya na wandugu zake mia mbili na makumi mbili chini ya usimamizi wake; Ukoo wa Gersoni: Yoeli na wandugu zake mia moja na makumi tatu chini ya usimamizi wake; Ukoo ya Elisafani: Semaya na wandugu zake mia mbili chini ya usimamizi wake; Ukoo wa Hebroni: Elieli na wandugu zake makumi munane chini ya usimamizi wake; Ukoo wa Uzieli: Aminadabu na wandugu zake mia moja kumi na wawili, chini ya usimamizi wake.


Hemani na Yedutuni walikuwa na baragumu na matoazi kwa ajili ya muziki na ala za muziki kwa ajili ya nyimbo takatifu. Wana wa Yedutuni walichaguliwa kwa kulinda milango.


Akamuchagua Asafu kuwa kiongozi wao, akisaidiwa na Zekaria. Yeieli, Semiramoti, Yehieli, Metitia, Eliabu, Benaya, Obedi-Edomu na Yehieli, akawachagua wakuwe wapiga vinanda na vinubi. Asafu alipiga matoazi,


elfu ine wakuwe walinzi wa milango, na elfu ine wakuwe waimbaji, wakimusifu Yawe kwa ala za muziki mufalme alizotengeneza mwenyewe kwa ajili ya kazi hiyo.


Kati ya watu wa ukoo wa Hebroni, Yeria alikuwa kiongozi wa ukoo na jamaa zote, na katika mwaka wa makumi ine wa utawala wa mufalme Daudi, uchunguzi ulifanywa na wanaume wenye uwezo mukubwa wakapatikana kule Yezeri katika jimbo la Gileadi.


Mufalme Hezekia alifuata maagizo ambayo Yawe alikuwa amemupa mufalme Daudi kwa njia ya Gadi, nabii wa mufalme na nabii Natani. Hivyo basi, akaweka Walawi katika nyumba ya Yawe, wamoja wao wakiwa na matoazi, wengine vinanda na wengine vinubi. Hiyo ilikuwa amri ya Yawe kwa njia ya manabii wake.


Kisha mufalme Hezekia na viongozi wakawaambia Walawi wamusifu Yawe kwa nyimbo ambazo mufalme Daudi na nabii Asafu walizotunga. Basi, watu wote wakamutukuza Mungu kwa furaha, na kuinama uso mpaka chini.


Waimbaji na wapiga baragumu wote pamoja walitoa sauti kwa pamoja na matoazi na vyombo vingine vya muziki, wakimusifu Yawe wakiimba: “Yeye ni muzuri. Wema wake unadumu milele.” Wakati ule nyumba ya Yawe ikajazwa na wingu.


Makuhani walikuwa wakisimama kwenye nafasi za kazi zao, nao Walawi, walisimama wakiwa na vyombo vya Yawe vya muziki mufalme Daudi alivyotengeneza kwa ajili ya kutoa shukrani kwa Yawe. Waliimba: “Wema wake unadumu milele.” Wakati Daudi alipotoa shukrani, walimusaidia; makuhani walipiga baragumu nao Waisraeli wote wakasimama.


Basi, watu wa Israeli, makuhani, Walawi na watu wengine waliokuwa wamerudi kutoka katika uhamisho wakaizindua nyumba ya Mungu kwa shangwe kubwa.


Watu wengine wa Israeli, makuhani na Walawi walikaa katika miji ya Yuda, kila mumoja katika urizi wake.


Siku hiyo, watu wakatoa sadaka nyingi na kufurahi maana Mungu aliwafanya kuwa na furaha kubwa. Vilevile wanawake na watoto, wote wakafurahi. Vigelegele vya furaha toka katika Yerusalema vikasikilika mbali.


Watu wote waliorudi kutoka katika uhamisho wakatengeneza vibanda wakaishi ndani yake. Hii ilikuwa ni mara ya kwanza watu kuishi katika vibanda tangu wakati Yesua mwana wa Nuni alipokuwa akiishi. Watu wakafurahi sana.


Mulisifu jina lake mukicheza, mumwimbie kwa ngoma na zeze.


Mashairi yanayoelekea muzinduo wa hekalu. Zaburi ya Daudi.


Mutafurahia mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi pamoja na wana wenu na wabinti zenu, watumishi wenu, Walawi, wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi pamoja nanyi. Mufanye haya katika pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kwa ajili ya jina lake.


“Kisha wakubwa watawaambia watu: ‘Kuna mutu yeyote hapa aliyejenga nyumba mupya lakini hajaizindua? Arudie kwake, kusudi asikufie kwenye vita na mutu mwingine aizindue.


Mufurahi siku zote katika kuungana kwenu na Bwana. Na tena ninasema: Mufurahi!


Wakati alipokuwa amekwisha kukamata kizingo, vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee makumi mbili na wane wakainama uso mpaka chini mbele ya Mwana-Kondoo. Kila mumoja wao alikuwa na kinubi na vikombe vya zahabu vilivyojaa marasi, ndiyo maombi ya watu wa Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ