Wakati wa Eliasibu, Yoyada, Yohanani na Yadua wakubwa wa jamaa za Walawi waliandikwa; vilevile wakati wa utawala wa mufalme Dario wakubwa wa jamaa za makuhani waliandikwa.
Viongozi wa Walawi Hasabia, Serebia, Yesua mwana wa Kadimieli walisimama kuelekeana na wandugu zao walipangwa kwa kuimba nyimbo za kusifu na kushukuru, kufuatana na amri ya mufalme Daudi, mutu wa Mungu.