Jamaa zingine za Walawi zilisimamia kazi ya nyimbo katika hekalu. Waliishi katika vyumba vimoja vya majengo ya nyumba ya Mungu na hawakuhitajika kufanya kazi ingine yoyote kwa maana walikuwa wakitumika usiku na muchana.
Watu wote wa Israeli, tangu wakati wa Zerubabeli na Nehemia, walitoa matoleo ya kila siku kwa ajili ya waimbaji na walinzi wa milango. Zaidi ya yote, watu wa Israeli wakatoa matoleo kwa ajili ya Walawi, nao Walawi wakatenga sehemu kwa ajili ya wazao wa Haruni.