Katika siku ya ine, tukiwa ndani ya nyumba ya Mungu wetu, tukapima ile feza, zahabu na vile vyombo, kisha tukavipatia kuhani Meremoti mwana wa Uria. Meremoti alikuwa pamoja na Eleazari mwana wa Finehasi, na Walawi wawili, Yozabadi mwana wa Yesua, na Noadia mwana wa Binui.
na Matania mwana wa Mika mwana wa Zabudi, wa uzao wa Asafu, aliyekuwa kiongozi wakati wa kuomba maombi ya shukrani. Bakubukia alikuwa musaidizi wake. Pamoja nao kulikuwa Abuda mwana wa Samua mwana wa Galali wa uzao wa Yedutuni.
Walawi hawa ndio walisaidia kuwaelewesha watu Sheria: Yesua, Bani, Serebia, Yamini, Akubu, Sabetayi, Hodia, Maasea, Kelita, Azaria, Yozabadi, Hanani na Pelaya; na kila mumoja akiwa akisimama pale alipokuwa.