Wakubwa hawa wa ukoo za baba zao, pamoja na wandugu zao walikuwa kwa jumla watu elfu moja na mia saba na makumi sita. Walikuwa wakubwa wenye uwezo mukubwa katika kazi yote ya nyumba ya Mungu.
vilevile wandugu zake waliokuwa wakubwa wa jamaa za baba zao; wote pamoja walikuwa watu mia mbili makumi ine na wawili. Vilevile kulikuwa Amasayi, mwana wa Azareli mwana wa Azayi mwana wa Mesilemoti mwana wa Imeri,
Kiongozi wa Walawi waliokaa Yerusalema alikuwa, Uzi, mwana wa Bani mwana wa Hasabia mwana wa Matania mwana wa Mika wa ukoo wa Asafu, waliokuwa waimbaji, viongozi waangalizi wa shuguli za nyumba ya Mungu.