Hivi, Waisraeli wote walihesabiwa kufuatana na vizazi vyao na kuandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda wamepelekwa katika utumwa mpaka Babeli kwa sababu ya kutokuwa waaminifu.
Amaria, Kuhani Mukubwa, ndiye atakayesimamia mambo yote yanayoelekea Yawe, naye Zebadia mwana wa Isimaeli, musimamizi wa inchi ya Yuda atasimamia mambo yote ya utawala, na Walawi watakuwa wakubwa. Mujipe moyo mutimize masharti haya, naye Yawe akuwe pamoja nao wanaokuwa wema.”
Nao Yehieli, Azazia, Nahati, Asaeli, Yeremoti, Yozabadi, Elieli. Isimakia, Mahati na Benaya, wakawekwa kuwa wasimamizi chini ya uongozi wa Konania na ndugu yake Simei. Hawa wote walichaguliwa na mufalme Hezekia, na Azaria, kuhani mukubwa wa nyumba ya Mungu.
pamoja na wandugu zao waliofanya kazi katika hekalu walikuwa mia nane makumi mbili na wawili. Pamoja na hao, kulikuwa Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia mwana wa Amsi mwana wa Zakaria mwana wa Pasuri mwana wa Malkiya;