Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 10:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 tunaungana na wandugu zetu, wakubwa wetu, katika kufanya kiapo na kwamba tukivunja kiapo hiki tutapata azabu, na tunaapa kwamba tutaishi kwa kufuata sheria ya Mungu ambayo alitoa kwa njia ya Musa, mutumishi wake; tena tutatii yote ambayo Yawe, Mungu wetu, anatuamuru; na kwamba tutashika maagizo na masharti yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 10:30
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mbele ya Yosia au nyuma yake hakuna mufalme yeyote aliyekuwa kama yeye, ambaye alimutumikia Yawe kwa moyo wake wote, kwa nguvu zake zote na kwa roho yake yote kulingana na Sheria ya Musa.


Halafu mufalme akasimama karibu na nguzo na kufanya agano mbele ya Yawe, kumufuata Yawe, kushika amri zake, maagizo na masharti yake kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, kutenda maneno yote ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hicho; nao watu wote wakaungana katika kufanya agano.


Kisha mufalme akasimama kwa pahali pake akafanya agano mbele ya Yawe, kumufuata Yawe, kushika amri, maamuzi na masharti yake kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, kutenda maneno yote ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki.


Kutokana na haya yote yaliyotokea, sisi tunaweka agano imara kwa maandiko na wakubwa wetu, Walawi na makuhani wanatia sahihi zao na muhuri wao.


Tena wakati ule nikaona Wayuda waliooa wanawake toka Asidodi, Amoni na Moabu;


Nikawakaripia na kuwalaani, hata nikawapiga wamoja kati yao na kuwaongoa nywele zao. Nikawalazimisha kuapa kwa jina la Mungu, nikisema: “Wabinti zenu musiwaoeshe kwa vijana wao, wala wabinti zao wasiolewe na vijana wenu au na ninyi wenyewe.


Nikawatakasa watu kutokana na chochote kilichokuwa cha kigeni. Nikatayarisha utaratibu kwa ajili ya makuhani na Walawi juu ya kazi ya kila mumoja wao.


Wao wakaitikia na kusema: “Tutawarudishia na hatutawadai chochote. Tutafanya kama vile ulivyosema.” Nikawaita makuhani mbele, na viongozi wote wakaapa mbele ya makuhani kufanya kama walivyoahidi.


Nimeapa na kuhakikisha kiapo changu, kwamba nitashika maamuzi yako ya haki.


Vijana wenu wakioa wabinti zao, na hao wabinti wanaoabudu miungu yao, watawashawishi vijana wenu kufuata miungu yao.


Muko hapa leo kwa kufanya agano pamoja na Yawe, Mungu wenu na kulihakikisha kwa kiapo.


Musioane nayo, wala musiyaoeshee wabinti zenu au wana wenu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ