Wana wa Hamu walikuwa baba za watu walioishi katika inchi ya Etiopia, Misri, Puti na Kanana. Wana wa Etiopia walikuwa: Seba, Havila, Sabuta, Rama na Sabuteka. Etiopia alizaa vilevile Nimurodi, aliyekuwa mutu shujaa wa kwanza katika dunia. Wana wa Rama walikuwa: Seba na Dedani.
akiwa na magari elfu moja na mia mbili, waaskari wapanda-farasi elfu makumi sita. Alikuwa vilevile na waaskari wengi sana wasioweza kuhesabiwa toka Misri; Walibia, Wasuki na Waetiopia.
Wale Waetiopia na Walibia hawakukuwa jeshi kubwa na magari na waaskari wapanda-farasi wengi? Lakini kwa vile ulimutegemea Yawe, yeye aliwatia katika mikono yako.
Musonge mbele, enyi farasi; mushambulie, enyi magari ya vita. Mashujaa wasonge mbele: watu wa Etiopia na Puti wanaoshika ngao, watu wa Ludi, wafundi wa kutumia pinde.
Watu kutoka Persia, Ludi na Puti walijiunga katika kundi lako la waaskari; walilundika ngao zao na kofia zao kwenye kambi zao za kiaskari. Waaskari hao walikupatia utukufu.