Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nahumu 1:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Yawe ni muzuri, yeye ni kimbilio la usalama wakati wa taabu. Yeye anawalinda wote wanaokimbilia usalama kwake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nahumu 1:7
53 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mumushukuru Yawe! Yeye ni muzuri, wema wake unadumu milele!


Waliweka tumaini lao kwa Mungu na wakamwomba awasaidie, naye akaitikia ombi lao na kuwatia katika mikono yao Wahagari pamoja na warafiki zao.


Kwa hiyo, watu wa Yuda walipata ushindi mbele ya Waisraeli kwa sababu walimutegemea Yawe, Mungu wa babu zao.


Si Hezekia ndiye anayewadanganya mukufe kwa njaa au kiu anapowaambia: ‘Yawe, Mungu wenu atawaokoa toka mikono ya mufalme wa Asuria?’


Naye Yawe akatuma malaika aliyewaua waaskari shujaa, majemadari na wakubwa katika kambi ya mufalme wa Asuria. Basi, mufalme wa Asuria akarudia katika inchi yake akijaa haya. Mara tu alipoingia ndani ya nyumba ya mungu wake, wana wake mwenyewe wakamwua palepale kwa upanga.


Yeye ana nguvu za kibinadamu tu, lakini sisi tuna Yawe, Mungu wetu, kwa kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Maneno haya ya mufalme Hezekia yakawatia moyo sana watu wale.


Wakaimba kwa kupokezana, wakimusifu na kumutukuza Yawe: “Yeye ni muzuri, wema wake kwa Waisraeli unadumu milele.” Watu wote walipaza sauti kwa nguvu zao zote, wakamusifu Yawe kwa sababu ya kuanza kujenga musingi wa nyumba ya Yawe.


Maana Yawe anashugulikia njia ya watu wa haki; lakini njia ya waovu itaangamia.


Yawe ni muzuri! Wema wake unadumu milele, na uaminifu wake kwa vizazi vyote.


Yawe ni muzuri na wa usawa, kwa hiyo anawafundisha wakosaji njia.


Siku ya taabu atanificha ndani ya nyumba yake; atanificha katika hema lake, atanilinda salama juu ya mulima.


Yawe anawaokoa watu wa haki, na kuwalinda wakati wa taabu.


Yawe anawasaidia na kuwaokoa; anawaopoa kutoka makucha ya waovu na kuwaokoa, maana wanakimbilia kwake.


Mungu ni kimbilio letu na nguvu yetu; yeye ni musaada wetu wakati wa taabu.


Uniite wakati wa taabu, nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”


Wanapitapita huko na huko wakitafuta chakula, nao wasiposhiba wananguruma.


Ukuwe kikingio changu cha kukimbilia, kimbilio lenye nguvu la kuniokoa, kwa maana wewe ni kikingio na kimbilio langu.


Siku za taabu ninakuita, maana wewe unaniitikia.


Yawe ni kikingio cha watu wanaoonewa; yeye ni kikingio katika nyakati za taabu.


Akiniita, mimi nitamwitikia; akikuwa katika taabu nitakuwa pamoja naye, nitamwokoa na kumupa heshima.


Jina la Yawe ni munara imara; mwenye haki anaukimbilia na kuwa salama.


Maana wewe umekuwa kimbilio kwa wazaifu, pango kwa wakosefu katika taabu zao. Wewe ni kimbilio wakati wa zoruba, kivuli wakati wa joto kali. Kweli pigo la watu wakali ni kali kama zoruba inayopiga ukuta;


Kila mumoja atakuwa kama pahali pa kujikinga na upepo, kama pahali pa kujificha wakati wa mvua kubwa. Watakuwa kama vijito vya maji katika inchi yenye kukauka, kama kivuli cha jiwe kubwa katika jangwa.


Nani kati yenu anayemwogopa Yawe? Nani anayetii maneno ya mutumishi wake? Kama kuna mutu anayetembea katika giza bila taa, amutumainie Yawe, na kumutegemea Mungu wake.


Ee Yawe! Wewe ndiwe nguvu yangu na upango wangu; wewe ni kimbilio langu wakati wa taabu. Mataifa toka pande zote za dunia yatakufikia na kusema: Miungu ya babu zetu ilikuwa ya uongo, ilikuwa ya bure, isiyofaa kitu.


Usiniletee hofu; maana wewe ndiwe kimbilio langu siku ya hasara.


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kama tini hizi zinavyokuwa nzuri, ndivyo nitakavyowaona kuwa wema watu wa Yuda ambao niliowaondoa toka nafasi hii na kuwapeleka katika uhamisho katika inchi ya Wababeli.


sauti za arusi na za furaha, sauti za waimbaji wakati wanaleta sadaka za shukrani katika nyumba ya Yawe. Wataimba hivi: Mumushukuru Yawe wa majeshi kwa sababu Yawe ni muzuri, kwa maana wema wake unadumu milele. Nitairudishia inchi hii hali yake ya zamani. –Ni Yawe anayesema.


Yawe ni muzuri kwa wanaomutegemea, kwa wote wanaomutafuta.


Basi, mufalme Nebukadneza akasema: Asifiwe Mungu wa Sadiraki, Mesaki na Abedenego kwa sababu alimutuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake ambao wanamutegemea. Wao walikataa kutii amri yangu ya kifalme, wakaitoa miili yao kama sadaka pahali pa kuabudu mungu mwingine, lakini Mungu wao peke yake.


Mungu wangu alileta malaika wake kwa kufunga vinywa vya simba hawa, nao hawakunizuru. Alifanya hivyo kwa sababu alijua mimi sina kosa lolote mbele yake na wala sijafanya jambo lolote baya mbele yako.


Nitakuachia watu wapole na wanyenyekevu ambao watakimbilia usalama kwangu mimi Yawe.


Yeye alimutumainia Mungu na alisema kwamba yeye ni Mwana wa Mungu. Ikiwa Mungu anapendezwa naye sasa amwokoe!”


Halafu mimi nitawaambia hivi waziwazi: ‘Sikuwajua ninyi hata siku moja. Mutoke karibu nami, ninyi watenda maovu.’


Mimi ni muchungaji mwema. Ninajua kondoo wangu na kondoo wangu wananijua,


Kondoo wangu wanasikia sauti yangu, ninawajua, nao wananifuata.


Basi ufikiri juu ya wema wa Mungu na ukali wake vilevile. Yeye ni mukali kwa wale walioanguka, lakini yeye ni mwema kwako, ikiwa utaendelea katika wema wake. Kama si vile, wewe vilevile utakatwa.


Lakini sasa munamujua Mungu, au afazali tuseme kwamba sasa munajulikana naye. Basi namna gani mumerudilia tena vitu vinavyotawala dunia, visivyokuwa na uwezo na vikosefu, mukitaka kuwa watumwa tena?


Lakini musingi uliojengwa na Mungu, unasimama imara. Nayo maneno haya yamechapwa juu ya musingi ule “Bwana anajua wale wanaokuwa wake,” na haya mengine: “Kila mutu anayesema kwamba yeye ni wa Bwana anapaswa kujitenga na maovu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ