Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 9:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Anayemwanga damu ya mwanadamu, damu yake itamwangwa na mwanadamu; maana mwanadamu aliumbwa kwa mufano wa Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 9:6
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Angalia, leo umenifukuza kutoka udongo wenye mboleo na mbali nawe. Basi, nitakuwa mukimbizi na mwenye kutangatanga katika dunia, na yeyote atakayeniona ataniua.”


Rubeni akawaambia: “Si niliwaambia tusimuzuru kijana? Lakini ninyi hamukunisikiliza! Sasa tunaazibiwa kwa ajili ya damu yake.”


Hiki ndicho kitabu cha uzao wa Adamu. Wakati Mungu alipowaumba wanadamu, aliwaumba kwa mufano wake.


Mutu mwovu anapomwua mutu wa haki akiwa katika kitanda ndani ya nyumba yake, basi si ni jambo la haki kwangu kumulipiza kwa sababu ya kumwanga damu kwa kumwondosha toka katika dunia?”


Lakini wewe usimwache bila kumwazibu. Una hekima, utajua utakalomufanyia. Ingawa yeye ana imvi, usimwache. Umwue ingawa ni muzee.”


Mara tu Atalia mama ya mufalme Ahazia alipoona kwamba mwana wake ameuawa, alitoka, akaangamiza watu wote wa jamaa ya kifalme.


Basi, wakamukamata, wakamupeleka na kumupitisha kwenye Mulango wa Farasi kuelekea nyumba ya kifalme, naye akauawa kule.


Kwa hiyo, watu wote walipata furaha na muji wote ulikuwa mutulivu, nyuma ya Atalia kuuawa kwa upanga katika nyumba ya kifalme.


Kisha watumishi wake walimufanyia shauri baya na kumwua katika nyumba yake ya kifalme.


Unisafishe kabisa kosa langu; unitakase zambi yangu.


Mutu anayelemewa na kosa ya kuua mutu, atakuwa mukimbizi mpaka katika kaburi. Mutu yeyote asijaribu kumusaidia.


wakati wa kuua na wakati wa kuponyesha, wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga,


bila kumuleta nyama huyo kwenye mulango wa hema la mukutano kwa kumutolea Yawe mbele ya makao yake, mutu yule atakuwa na kosa ya kumwanga damu. Amemwanga damu na atatengwa na watu wake.


Mutu yeyote anayeua mutu mwingine anapaswa naye kuuawa.


Lakini mutu akimupiga mwenzake kwa kitu cha chuma, na kumwua, mutu huyo ni mwuaji na anapaswa kuuawa.


Baraza litamwokoa mutu huyo aliyeua toka katika mikono ya ndugu ya mutu aliyeuawa, na kumurudisha katika muji wa makimbilio alimokuwa amekimbilia. Atakaa huko mpaka kufa kwa Kuhani Mukubwa wa wakati ule aliyechaguliwa kwa kupakwa mafuta matakatifu.


Mukifanya hivyo mutachafua inchi ambayo munakaa ndani yake. Umwangaji wa damu unachafua inchi, na hakuna sadaka inayoweza kutakasa inchi iliyofanyiwa mauaji isipokuwa kwa kumwua mwuaji huyo.


Halafu Yesu akamwambia: “Rudisha upanga wako katika kifuko chake, kwa maana yeyote anayetumia upanga, atauawa kwa upanga.


maana yeye anamutumikia Mungu kwa faida yako. Lakini kama ukifanya mabaya, umwogope kwa sababu yeye yuko na uwezo kwa kuazibu. Yeye anamutumikia Mungu wa kuazibu wale wanaofanya mabaya.


Mwanaume hapaswi kufunika kichwa, kwa sababu yeye ni mufano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamuke ni utukufu wa mwanaume.


“Lakini mutu akiwa adui wa mwenzake, akivizia, akimushambulia na kumwua, kisha anakimbilia kwenye muji mumoja wa miji hiyo,


Kwa njia ya ulimi tunamusifu Bwana anayekuwa Baba yetu, na kwa njia ile ile tunalaani watu walioumbwa kwa mufano wa Mungu.


Mutu yule aliyekusudiwa kuwa mufungwa, atafungwa; na yule aliyekusudiwa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Kwa sababu hiyo, watu wa Mungu wanapaswa kuwa wavumilivu na wenye imani.”


Hivi ndivyo Mungu alivyomwazibu Abimeleki kwa kosa lake juu ya baba yake kwa kuwaua wandugu zake makumi saba.


Samweli akasema: “Kwa sababu upanga wako umewafanya wamama wengi wasikuwe na watoto, ndivyo na mama yako atakavyokuwa bila mutoto kati ya wamama.” Akamukatakata Agagi vipandevipande mbele ya Yawe kule Gilgali.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ