Basi, uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninyi munakula nyama yenye damu, munaziabudu sanamu za miungu yenu na kumwanga damu! Munazani kwamba mutapewa inchi hii ikuwe yenu?
Lakini inafaa tuwaandikie kwa kuwaambia kwamba wajitenge na vitu vilivyochafuliwa kwa kutambikia sanamu, waepuke uasherati na wasikule nyamafu wala damu.
Kwa sababu hii sisi tumekata shauri kwa nia moja, tukapatana kuchagua watu wamoja na kuwatuma kwenu. Watu hawa watawafikia pamoja na wapendwa wetu, Barnaba na Paulo,
musikule vyakula vilivyotolewa kwa kutambikia sanamu; musikule damu wala nyamafu; na muepuke uasherati. Mutafanya vema kama mukijitenga na mambo haya. Salamu kwenu.”
Musikule nyamafu yeyote lakini munaweza kumupa mugeni anayeishi katika miji yenu, akule, au munaweza kumwuzishia mutu wa taifa lingine. Musipike mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake. “Ninyi ni watakatifu na Yawe ni Mungu wenu.