Lakini Semu na Yafeti wakatwaa nguo, wakaiweka juu ya mabega yao, wakakwenda kinyumenyume na kufunika uchi wa baba yao. Waliangalia pembeni, wala hawakuuona uchi wa baba yao.
Wana wa Hamu walikuwa baba za watu walioishi katika inchi ya Etiopia, Misri, Puti na Kanana. Wana wa Etiopia walikuwa: Seba, Havila, Sabuta, Rama na Sabuteka. Etiopia alizaa vilevile Nimurodi, aliyekuwa mutu shujaa wa kwanza katika dunia. Wana wa Rama walikuwa: Seba na Dedani.
Wandugu zangu, kama mutu akipatikana na kosa fulani, ninyi munaoongozwa na Roho wa Mungu mumwonye mutu yule kwa roho ya upole. Na kila mumoja wenu ajiangalie mwenyewe, kusudi asijaribiwe vilevile.