Yawe, yule aliyepanga jua liangaze muchana, mwezi na nyota viangaze usiku, na anayevumisha mawimbi ndani ya bahari, yule ambaye jina lake ni Yawe wa majeshi, anasema hivi:
Wala hawasemi wenyewe hivi: Inatupasa kumwogopa Yawe, Mungu wetu, anayetujalia mvua kwa wakati wake, anayetupatia mvua za kwanza na mvua za mwisho; na kutupatia nyakati nzuri za mavuno.
Basi wandugu, muvumilie mpaka Bwana atakaporudia. Muangalie namna mulimaji anavyongojea shamba litoe mavuno yanayokuwa ya faida kubwa. Yeye anavumilia mpaka wakati mvua ya kwanza na ya mwisho zinaponyesha.