Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 8:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kisha Mungu akamukumbuka Noa na nyama wote wa pori na wa kufugwa waliokuwa pamoja naye ndani ya chombo. Basi, Mungu akavumisha upepo juu ya inchi, maji yakaanza kupunguka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 8:1
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu alipoangamiza miji katika bonde ambamo Loti alikuwa anakaa, alimukumbuka Abrahamu kwa kumutosha Loti katika miji hiyo, kusudi Loti asiangamizwe pamoja nayo.


Kisha Mungu akamukumbuka Rakeli, akakubali ombi lake na kumujalia kupata watoto.


na viumbe vyote vyenye uzima, ndege, nyama wa kufugwa na wa pori, wote waliotoka katika chombo pamoja nanyi.


Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa ajili ya haya yote na usiyasahau matendo yangu mema niliyofanya kwa ajili ya nyumba yako na kwa ajili ya kazi yako.


Nikaagiza Walawi kujitakasa na kwenda kulinda milango kwa kutakasa siku ya Sabato. Ee, Mungu wangu, unikumbuke hata na kwa hili vilevile unihurumie kutokana na rehema zako kubwa.


Ee Mungu, kumbuka jinsi watu walivyochafua ukuhani na agano la kikuhani na la Walawi.


Nikaagiza matoleo ya kuni kufanyika katika wakati unaopaswa na malimbuko wakati wake. Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa ajili ya haya yote na unijalie mema.


Akizuia mvua, inchi inakauka; akiifungulia, inchi inaharibika.


Heri ungenificha katika kuzimu, ungenificha mpaka kasirani yako itulie, nawe ungenipimia muda kwa kunikumbuka tena.


Alikumbuka ahadi yake takatifu aliyomupa Abrahamu mutumishi wake.


Unikumbuke, ee Yawe, unapowaonyesha watu wako upendo. Unisaidie wakati unapowaokoa,


Yawe anatukumbuka na atatubariki. Atawabariki watu wa Israeli, atawabariki wazao wa Haruni,


Wimbo wa safari za kidini. Ee Yawe, umukumbuke Daudi, kumbuka taabu zote alizopata.


Alitukumbuka wakati wa uzaifu wetu. Wema wake unadumu milele.


Ee Yawe, usisahau mambo Waedomu waliyotenda, siku ile Yerusalema iliponyanganywa; kumbuka maneno haya waliyosema: “Mubomoe Yerusalema! Muongoe hata na misingi yake!”


Yawe ameikaa juu ya mafuriko ya maji; Yawe ni mufalme anayetawala milele.


Wema wako, ee Yawe, unaenea hata mbinguni; uaminifu wako unafika hata kwenye mawingu.


Musa akanyoosha mukono wake juu ya bahari, naye Yawe akasukuma bahari nyuma kwa upepo mukali toka upande wa mashariki. Upepo ule ulivuma usiku kucha, ukagawanya bahari sehemu mbili na katikati kukatokea inchi kavu.


Lakini wewe uliuvumisha upepo wako, nayo bahari ikawafunika. Walizama ndani ya maji kama risasi.


Mungu akasikia kilio chao, naye akakumbuka agano alilofanya na Abrahamu, Isaka, na Yakobo.


Upepo wa kaskazini unaleta mvua; vilevile mwenye kusingiziana analeta chuki.


Mimi ndiye ninayeviamuru vilindi: Mukauke, nitakausha mito yenu.


Jua kali liyapige maji, kusudi yapate kukauka! Maana Babeli ni inchi inayojaa sanamu za miungu, watu ni wenda-wazimu kwa sababu ya miungu yao.


Yawe, utukufu wa Yakobo, ameapa: Hakika, sitayasahau matendo yao maovu.


Basi, haifai kwangu kuuhurumia Ninawe, ule muji mukubwa wenye watu elfu mia moja na makumi mbili, wasioweza kutambua linalokuwa jema na baya; na nyama wengi wasiokuwa na hesabu?


Anaikaripia bahari na kuikausha, yeye anaikausha mito yote. Mbuga za Basani na mulima Karmeli zinanyauka, maua ya Lebanoni yanakauka.


Ee Yawe, nimesikia juu ya utukufu wako, juu ya matendo yako, nami ninaogopa. Uyafanye tena mambo yale wakati wetu; uyafanye yajulikane wakati huu wetu. Unapokasirika tafazali ukumbuke huruma yako!


Watapitia katika bahari ya mateso, nami nitayapiga mawimbi yake, na vilindi vya maji ya muto Nili vitakauka. Kiburi cha Asuria kitavunjwa na nguvu za Misri zitatoweka.


Wakati wa vita katika inchi yenu juu ya waadui wanaowashambulia, mutatoa kitambulisho cha vita kwa kupiga baragumu hizi kusudi Yawe, Mungu wenu apate kuwakumbuka na kuwaokoa na waadui zenu.


Malaika wa Yawe akamwambia Balamu: Mbona umemupiga punda wako mara tatu? Nimekuja kukuzuia, kwa sababu njia yako ni mbaya.


Na ule muji mukubwa ukagawanyika katika sehemu tatu, na miji ya mataifa yote ikabomoka. Mungu hakusahau muji mukubwa Babeli, akaukunywesha kikombe kinachokuwa na divai ya kasirani yake kali.


Kwa maana zambi zake zinazidi sana hata zimefika mbinguni na Mungu hakusahau mabaya yake.


Kesho yake asubui, Elekana na jamaa yake waliamuka asubui mapema, na kisha kumwabudu Yawe, walirudi kwao Rama. Elekana akalala na muke wake Hana na Yawe akamukumbuka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ