Noa alipokuwa na umri wa miaka mia sita, katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili, siku hiyo chemichemi zote za vilindi vya udongo zikabubujika maji, na madirisha ya mbinguni yakafunguka.
Noa alipokuwa na umri wa miaka mia sita na moja, siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, maji yalikuwa yamekauka katika inchi. Noa akafunua kifuniko cha chombo, na alipoangalia, akaona kwamba inchi ilikuwa imekauka.