5 Noa akafanya yote kama vile Yawe alivyomwamuru.
Noa akafanya yote kama vile Mungu alivyomwamuru.
Kila aina yao waliingia dume na dike kama vile Mungu alivyomwamuru Noa. Kisha, Yawe akafunga mulango wa chombo nyuma ya Noa.
Nikichunguza amri zako zote, hapo kweli sitapata haya.
Basi, kazi yote ya hema la mukutano ikamalizika. Waisraeli walifanya yote kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
Basi, Musa alitimiza kwa ukamilifu kabisa maagizo yote ya Yawe.
Basi, Musa na Haruni wakafanya hivyo. Hakika, walifanya kama vile Yawe alivyowaamuru.
Lakini Yesu akamujibu: “Ukubali kufanya hivi sasa. Kwa maana ni kwa njia hii tutatimiza mambo yote yanayokuwa ya haki mbele ya Mungu.” Basi Yoane akakubali.
Lakini Yesu akawajibu: “Mama yangu na wandugu zangu ni wale wanaosikia neno la Mungu na kulishika.”
Sasa kwa kuona munajua jambo hili, mutakuwa wenye heri kama mukilifanya.
Halafu mama yake akawaambia watumishi: “Mufanye kila kitu atakachowaambia.”
Alijinyenyekeza na kutii mpaka kufa, ndiko kufa kwake juu ya musalaba.
Ijapokuwa alikuwa Mwana wa Mungu, alijifunza kutii kwa njia ya mateso yale aliyopata.