Utwae pamoja nawe nyama wote wanaohesabiwa kuwa safi, dume saba na dike saba ya kila aina. Lakini nyama wanaohesabiwa kuwa wachafu, utwae dume na dike ya kila aina.
Nyuma ya siku saba, nitanyesha mvua juu ya inchi siku makumi ine muchana na usiku, na kila kiumbe chenye uzima nilichokiumba katika dunia nitakiangamiza.”
Noa akamujengea Yawe mazabahu, akatwaa mumoja katika kila aina ya nyama wanaohesabiwa kuwa safi na ndege anayehesabiwa kuwa safi, akamutolea Mungu sadaka za kuteketezwa kwa moto juu ya mazabahu.