Nyuma ya siku saba, nitanyesha mvua juu ya inchi siku makumi ine muchana na usiku, na kila kiumbe chenye uzima nilichokiumba katika dunia nitakiangamiza.”
Elia akaamuka, akakula na kunywa. Kisha akatembea kwa nguvu ya chakula hicho mwendo wa siku makumi ine, muchana na usiku, mpaka Horebu kwenye mulima wa Mungu.
“Nikakaa kwenye mulima kwa muda wa siku makumi ine, usiku na muchana, kama vile mbele. Yawe akanisikiliza kwa mara ingine tena na akakubali kutowaangamiza.
Kisha nikalala uso mpaka chini mbele ya Yawe, kama vile mbele, kwa muda wa siku makumi ine usiku na muchana. Sikukula chakula wala kunywa maji, kwa sababu ya zambi muliyokuwa mumetenda kwa kufanya maovu mbele ya Yawe kwa kumukasirikisha.
Nilipopanda juu ya mulima kupokea vibao vya mawe ambavyo kuliandikwa agano ambalo Yawe alifanya nanyi, nilikaa huko siku makumi ine, usiku na muchana; sikukula wala kunywa chochote.