Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 7:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Noa alipokuwa na umri wa miaka mia sita, katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili, siku hiyo chemichemi zote za vilindi vya udongo zikabubujika maji, na madirisha ya mbinguni yakafunguka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 7:11
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ikakuwa hivyo. Mungu akafanya anga, akatenga maji yanayokuwa juu ya anga na yale yanayokuwa chini ya anga lile.


Nitaleta mafuriko ya maji kwa kuangamiza viumbe vyote vyenye uzima katika dunia. Kila kiumbe chenye uzima katika dunia kitakufa.


Noa alikuwa na umri wa miaka mia sita wakati mafuriko ya maji yalipotokea juu ya inchi.


Siku ya makumi mbili na saba ya mwezi wa pili, inchi ilikuwa imekauka kabisa.


Chemichemi za maji ya vilindi na madirisha ya mbinguni yakafungwa. Mvua ikazuiwa,


Yule jemedari mulinzi wa mufalme alikuwa amemwambia Elisha: “Hata kama Yawe mwenyewe angefanya madirisha mbinguni, jambo hilo litawezekana?” Naye Elisha alikuwa amemujibu: “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hautakula.”


Jemedari mulinzi wa mufalme akamwambia Elisha: “Hata kama Yawe mwenyewe angefanya madirisha mbinguni, jambo hilo litawezekana?” Elisha akamujibu: “Utaona kwa macho yako mwenyewe, lakini wewe hautakula.”


Akizuia mvua, inchi inakauka; akiifungulia, inchi inaharibika.


Mwanadamu anachimba mashimo mbali na makao ya watu, mbali na watu pahali kusipofikiwa, wachimba madini wananinginia wakifungwa kamba.


Umepata kufika kwenye chemichemi za bahari au kutembea juu ya sakafu ya kilindi cha bahari?


Nani mwenye akili ya kuweza kuhesabu mawingu au kuinamisha vibuyu vya maji kule katika mbingu


Alikusanya maji ya bahari kama katika chupa, akavifunga vilindi vya bahari ndani ya gala.


Wewe umefanya chemichemi na vijito; na kukausha mito mikubwa.


Kwa maarifa yake vilindi vilipasuka, na mawingu yakadondosha umande.


Mutu atakayekimbia sauti ya woga atatumbukia ndani ya shimo; na mutu atakayetoka ndani ya shimo atanaswa katika mutego. Madirisha ya mbinguni yamefunguliwa, misingi ya dunia inatikisika.


Dunia inavunjikavunjika, inapasuka na kutikiswatikiswa.


Mbona hamuniogopi? –Ni ujumbe wa Yawe.– Kwa nini hamutetemeki mbele yangu? Mimi niliwekea bahari muchanga kuwa mupaka wake; ni kizuizo cha milele ambacho bahari haiwezi kuvuka. Ingawa mawimbi yanaupiga, hayawezi kuupita; ingawa yanavuma, hayawezi kuuruka.


Anapotoa sauti yake maji yanajikusanya mbinguni, anafanya ukungu upande kutoka mipaka ya dunia. Anafanya umeme upige wakati wa mvua, anavumisha upepo kutoka gala zake.


Maana, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitakufanya wewe Tiro kuwa matongo, kama miji isiyokuwa na watu, nitakapoleta juu yako maji kutoka vilindi vya bahari, na maji mengi yatakufunika.


Mulete katika gala yangu zaka yote, kusudi katika nyumba yangu kuwe chakula cha kutosha. Kisha munaweza kunijaribu. Munipime namna hiyo nanyi mutaona kama sitayafungua madirisha ya mbinguni na kuwatiririshia baraka tele.


Kwa maana katika siku zile mbele ya kunyesha kwa mvua kubwa, watu walikuwa wakikula na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka ilipotimia siku ile Noa alipoingia ndani ya chombo.


Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.


Vilevile kufuatana na ile, dunia ya zamani iliangamizwa kwa mafuriko ya maji.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ