Wakati Abramu alipokuwa na umri wa miaka makumi tisa na tisa, Yawe akamutokea, akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Uwezo. Uendelee mbele yangu na kuwa mukamilifu.
Kisha Israeli akamubariki Yosefu, akisema: “Mungu ambaye babu zangu Abrahamu na Isaka walimutii katika maisha yao, Mungu ambaye ameniongoza katika maisha yangu mpaka leo,
Yawe akamwambia Noa: “Ingia ndani ya chombo wewe pamoja na jamaa yako yote, kwa maana, kati ya watu wote wa kizazi hiki, nimekuona wewe peke yako kuwa mutu wa haki mbele yangu.
Solomono akamwambia: “Ulimwonyesha wema mwingi mutumishi wako Daudi, baba yangu, kwa sababu alikutumikia kwa uaminifu, kwa haki na kwa moyo wa usawa; na umedumisha mema yako kwa kumupa mwana anayeikaa sasa kwenye kiti chake cha kifalme.
Yawe akamwambia Shetani: “Umemwona vizuri mutumishi wangu Yobu? Katika dunia hakuna mwingine anayekuwa kama yeye. Yeye ni mutu mukamilifu, wa usawa, mwenye kumwogopa Mungu na mwenye kuepukana na uovu.”
Hata kama Noa, Danieli na Yobu wangalikuwa ndani ya inchi ile, wangeyaokoa tu maisha yao wenyewe kwa ajili ya haki yao. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
Na hata kama Noa, Daneli na Yobu wangelikuwa ndani ya inchi ile, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– hawangeweza kuwaokoa hata mwana au binti. Wangeyaokoa tu maisha yao wenyewe kwa ajili ya haki yao.
Wakati ule katika Yerusalema kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Simeoni. Mutu huyo alikuwa mwenye haki na mwenye kuogopa Mungu. Alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa taifa la Israeli. Roho Mutakatifu alikuwa pamoja naye;
Kulikuwa mutu mumoja muzaliwa wa Arimatea, katika jimbo la Yuda, jina lake lilikuwa Yosefu. Mutu huyu alikuwa mwema na mwenye haki, naye alikuwa akitazamia Ufalme wa Mungu. Yeye alikuwa mumoja wa washauri wa Baraza Kubwa, lakini hakukubali shauri na matendo ya wenzake.
Nao wakamujibu: “Tumetumwa hapa na Kornelio, mukubwa wa waaskari. Yeye ni mutu wa haki na mwenye kumutii Mungu, naye anasifiwa na Wayuda wote. Malaika mutakatifu amemutokea na kumwagiza akuite ufike kwake kusudi asikie maneno utakayomwambia.”
Kwa maana Habari Njema inaonyesha namna Mungu anavyowahesabia watu haki mbele yake. Jambo hilo haliwezekani isipokuwa kwa njia ya kuamini tu. Ni sawa vile inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu yanayosema: “Mwenye haki ataishi kwa njia ya imani.”
Na zaidi ya hii ni wazi kwamba hakuna mutu anayehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya Sheria. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mwenye haki ataishi kwa njia ya imani.”
Kwa njia ya imani, Noa alionywa na Mungu juu ya mambo yatakayotokea, yale aliyokuwa hajayaona bado. Yeye alimutii Mungu na kujenga chombo kwa kujiokoa yeye mwenyewe pamoja na jamaa yake. Kutokana na hayo yote akahukumu dunia na kupokea haki inayopatikana kwa njia ya imani.
Nanyi vilevile, kama mawe yenye uzima mutumiwe kwa kujenga hekalu la kiroho. Na mule mutafanya kazi takatifu ya ukuhani kwa kutoa sadaka za kiroho zinazomupendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.
Mungu hakuhurumia dunia ya zamani, lakini alimulinda Noa, muhubiri wa haki, pamoja na watu wengine saba alipoleta mafuriko ya maji juu ya dunia ile ya waovu.