Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 6:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Lakini Noa akapata kukubaliwa mbele ya Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 6:8
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ni kweli kwamba mimi mutumishi wako nimepata kukubaliwa mbele yako, nawe umenitendea mema sana kwa kuokoa maisha yangu. Lakini kwenye milima ni mbali sana. Maangamizi haya yatanikuta mbele sijafika kule, nami nitakufa.


Yawe anawalinda wote wanaomupenda; lakini anawaangamiza waovu wote.


Siku moja tu ndani ya hekalu lako, ni bora kuliko siku elfu pahali pengine; afazali kubakia kwa mulango wa nyumba yako, kuliko kuishi ndani ya nyumba ya waovu.


Mutu muzuri anapata rehema za Yawe, lakini mwenye nia mbaya analaaniwa na Mungu.


Hivyo utakubaliwa na kusifiwa, mbele ya Mungu na mbele ya wanadamu.


Anayenipata mimi amepata uzima, na upendeleo kutoka kwa Yawe.


Yawe anasema hivi: Watu walioponyoka kuuawa, nilionyesha neema yangu kwao katika jangwa. Wakati Israeli alipotafuta kwenda kupumzika,


Hata kama Noa, Danieli na Yobu wangalikuwa ndani ya inchi ile, wangeyaokoa tu maisha yao wenyewe kwa ajili ya haki yao. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Kama ilivyokuwa katika siku za Noa, ndivyo itakavyokuwa wakati Mwana wa Mutu atakaporudi.


Halafu malaika akamwambia: “Maria, usiogope, kwa maana Mungu amekujalia neema.


Na kama ilivyokuwa katika siku za Noa, ni vile itakavyokuwa katika nyakati za kuja kwa Mwana wa Mutu.


Mungu akamujalia Daudi neema hata akamwomba yeye Mungu wa Yakobo ruhusa ya kumujengea nyumba.


Na ikiwa walichaguliwa kwa neema ya Mungu, si kufuatana na matendo. Ingekuwa vile, neema isingekuwa neema tena.


Mutu anayefanya kazi, mushahara wake hauhesabiwi kama zawadi, lakini ni haki yake.


Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa sawa hivi ninavyokuwa, na neema yake niliyopewa haikukuwa ya bure, lakini nilitumika zaidi sana kuliko mitume wote wengine. Hakika si mimi, lakini ni neema ya Mungu inayokuwa pamoja nami.


Lakini, Mungu aliyenichagua mbele sijazaliwa na kuniita kwa neema yake, alipendezwa


Bwana amusikilie huruma kwa Siku ile! Unajua vizuri sana vilevile mambo yote aliyonitendea kule Efeso.


Kwa maana neema ya Mungu inayoleta wokovu kwa watu wote imeonekana waziwazi.


Ilifanyika vile, kusudi kwa neema yake tupate kuhesabiwa haki mbele ya Mungu na kuupata uzima wa milele tunaotumainia.


Kwa sababu hii, tujongelee kwa uhodari kiti cha kifalme cha Mungu pahali anapowajalia watu neema kusudi apate kutuhurumia na kutujalia neema ya kutusaidia kwa wakati unaofaa.


Roho zile ni za watu walioasi Mungu zamani za kale alipowavumilia katika siku Noa alipotengeneza chombo kikubwa. Ni watu wanane tu ndio waliingia ndani ya chombo na kuokolewa katika maji.


Mungu hakuhurumia dunia ya zamani, lakini alimulinda Noa, muhubiri wa haki, pamoja na watu wengine saba alipoleta mafuriko ya maji juu ya dunia ile ya waovu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ