Utakitengeneza hivi: urefu wake metre mia moja makumi tatu na tatu, upana wake metre makumi mbili na mbili na urefu wake kwenda juu metre kumi na tatu.
Lakini kwa vile hakuweza kumuficha zaidi ya muda ule, akatengeneza namna ya kikapu cha mafunjo, akakipakaa namna ya kabulimbo, akamutia yule mutoto ndani. Kisha akaweka kikapu kando ya muto Nili katika majani.
Kwa maana katika siku zile mbele ya kunyesha kwa mvua kubwa, watu walikuwa wakikula na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka ilipotimia siku ile Noa alipoingia ndani ya chombo.
Siku zile watu walikuwa wakikula na kunywa, wakioa na kuolewa mpaka ilipotimia siku ile Noa alipoingia ndani ya chombo. Halafu mvua kubwa ikanyesha na kuwaangamiza wote.
Roho zile ni za watu walioasi Mungu zamani za kale alipowavumilia katika siku Noa alipotengeneza chombo kikubwa. Ni watu wanane tu ndio waliingia ndani ya chombo na kuokolewa katika maji.