Yawe akamwambia Noa: “Ingia ndani ya chombo wewe pamoja na jamaa yako yote, kwa maana, kati ya watu wote wa kizazi hiki, nimekuona wewe peke yako kuwa mutu wa haki mbele yangu.
kwa sababu umetubu na kunyenyekea mbele yangu, hata umepasua nguo yako na kulia uliposikia maneno yangu juu ya pahali hapa, na juu ya wakaaji wake, na umejinyenyekeza mbele yangu, nami vilevile nimekusikia. –Ni ujumbe wa Yawe.–
Mateso makali hayatasikilika tena katika inchi yako; wala uharibifu na maangamizi ndani ya mipaka yako. Utaweza kuziita kuta zako: “Wokovu”, na milango yako: “Sifa”.
Kama vile maji yanavyotiririka toka ndani ya kisima, ndivyo maovu yanavyotiririka katika Yerusalema. Mateso makali na maangamizi yanasikilika ndani yake. Ninaona magonjwa na vidonda mbele yangu kila siku.
Ustawi wa biashara yako ulikujaza ukali, ukatenda zambi. Kwa hiyo nilikufukuza kama muchafu, mbali na mulima wangu mutakatifu. Na yule kerubi aliyekulinda akakufukuzia mbali na mawe yanayometameta.
Mungu akaniambia: Wewe mwanadamu, umeyaona mambo hayo? Hata hivyo, watu wa Yuda wanaona machukizo hayo kuwa ni kidogo. Wanajaza mateso makali katika inchi na kuzidi kunikasirikisha. Angalia jinsi wananichukiza!
Mateso uliyoyatenda kule Lebanoni yatakulemea wewe; uliwaua nyama, nyama nao watakuogopesha. Yote hayo yatakupata wewe, kwa mauaji na mateso uliyoitendea dunia, uliyoifanyia miji na wakaaji wake wote.
Wewe umenyanganya mataifa mengi, lakini wote wanaobaki watakunyanganya wewe, kwa mauaji na mateso uliyoitendea dunia, uliyoifanyia miji na wakaaji wake wote.
Basi tunajua kama maneno yote yanayosemwa na Sheria, yanawaelekea wale wanaolazimishwa kutii Sheria, kusudi mutu yeyote asikuwe na namna ya kujitetea, na dunia nzima ipaswe kuhukumiwa na Mungu.
Maana ninajua kwamba nyuma ya kifo changu hakika mutakuwa waovu na kuacha ile njia niliyowaamuru muifuate. Na katika siku zinazokuja mutapatwa na hasara kwa sababu mutafanya maovu mbele ya Yawe na kumukasirikisha kwa matendo yenu.”
Lakini kila mara mwamuzi alipokufa walirudilia mienendo yao ya zamani, wakaishi vibaya kuliko babu zao. Waliifuata miungu mingine, wakaitumikia na kuinama mbele yao, wala hawakuyaacha matendo yao wala uasi wao.