Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 50:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Kisha Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi sasa ninakaribia kufa. Lakini Mungu hakika atawafikia kwa kuwasaidia. Atawatoa katika inchi hii na kuwapeleka katika inchi aliyowaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 50:24
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Inchi niliyowapa Abrahamu na Isaka nitakupa wewe na wazao wako.”


Ukae katika inchi hiyo, nami nitakuwa pamoja nawe na kukubariki. Nitatimiza ahadi niliyomupa baba yako Abrahamu, maana nitakupa wewe na wazao wako inchi hizi zote.


Yawe alisimama juu ya ngazi hiyo, akamwambia: “Mimi ni Yawe, Mungu wa Abrahamu baba yako, na Mungu wa Isaka. Nitakupa inchi unayoilalia wewe na wazao wako.


Kisha Israeli akamwambia Yosefu: “Kama vile unavyoona, mimi niko karibu kufa. Hata hivyo, Mungu atakuwa pamoja nanyi, na kuwarudisha katika inchi ya babu zenu.


Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nawe kule Misri na kukurudisha huku. Utakapokufa, mukono wa Yosefu ndio utakaofumba macho yako.”


Siku hiyo, Yawe akafanya agano na Abramu akisema: “Ninawapa wazao wako inchi hii, toka muto Nili wa Misri mpaka ule muto mukubwa wa Furati,


Yawe akamwambia Abramu: “Mimi ni Yawe niliyekuleta toka Uri, muji wa Wakaldea, kusudi nikupe inchi hii uirizi.”


Basi, simama uitembelee inchi hii katika upana na urefu, maana nitakupa wewe inchi ile.”


Inchi hii yote unayoona nitakupa wewe na wazao wako ikuwe yenu milele.


Halafu Yawe akamutokea Abramu, akamwambia: “Nitawapa wazao wako inchi hii.” Basi, Abramu akajenga mazabahu kwa ajili ya Yawe aliyemutokea.


Kwa njia ya imani, Yosefu alipokuwa karibu kufa, alisema juu ya habari za wakati Waisraeli watakapotoka katika inchi ya Misri, na kuwaagiza juu ya mifupa yake.


Kila mutu anapaswa kufa mara moja tu, na nyuma ya kufa, anahukumiwa na Mungu.


Kwa njia ya mutu mumoja zambi iliingia katika dunia, nayo zambi ikaleta kifo. Ni hivi vilevile kifo kimefikia watu wote, kwa sababu wote wamefanya zambi.


mavumbi yanarudilia inchi tena, na roho inamurudilia Mungu aliyeipana.


watu wanaogopa mupando na kutishwa katika njia, muti wa lozi unachanua maua yake meupe, mapanzi hayawezi kuruka, hakuna hamu tena, mwanadamu anaelekea kwenye makao yake ya milele, waombolezaji wanasambaa katika njia,


Kweli! Ninajua utanipeleka tu katika kifo, pahali wote wanaoishi watakapokutana.


“Kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyowaapia babu zenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo, yeye atawapa inchi yenye miji mikubwa na mizuri iliyostawi ambayo ninyi hamukuijenga.


Inchi hii yote nimeiweka mbele yenu. Basi, muende kutwaa inchi hiyo ambayo mimi Yawe niliapa kuwapa wazee wenu Abrahamu, Isaka, Yakobo na wazao wao.’ ”


Hakika hakuna mutu yeyote kati ya watu waliotoka Misri mwenye umri wa miaka makumi mbili na zaidi atakayeona inchi niliyoapa kuwapa Abrahamu, Isaka na Yakobo, kwa sababu hawakunitii kwa ukamilifu.


Yawe akamwambia Musa: Anza safari uondoke hapa, wewe na watu hao uliowatoa katika inchi ya Misri. Muende katika inchi niliyowapia Abrahamu, Isaka na Yakobo, nikisema: Nitawapa wazao wenu inchi hii.


Watu wakaamini. Na waliposikia kwamba Yawe amekuja kuwasaidia Waisraeli na kwamba ameyaona mateso yao, wote wakainamisha vichwa vyao na kumwabudu.


‘Mimi niko karibu kufa. Inakupasa kunizika katika kaburi nililojichongea katika inchi ya Kanana.’ Kwa hiyo ninamwomba aniruhusu niende kumuzika baba yangu, kisha nitarudi.”


Yawe akamukumbuka Sara, akamutendea kama alivyoahidi.


Nitakupa wewe na wazao wako inchi hii ambamo unaishi kama mugeni. Ni kusema inchi yote ya Kanana ikuwe mali yenu milele; nami nitakuwa Mungu wao.”


Kwa jasho la uso wako utajipatia chakula, mpaka utakaporudi katika udongo, maana ulitwaliwa katika udongo. Wewe ni mavumbi na utarudi katika mavumbi.”


Lakini Abramu akamwambia: “Ee Yawe, nitajua namna gani kwamba nitarizi inchi hii?”


na hivyo, nimeshuka kusudi niwaokoe toka mikono ya Wamisri. Nitawatoa katika inchi na kuwapeleka katika inchi nzuri na kubwa, inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.


Musa alipeleka mifupa ya Yosefu kama vile Yosefu alivyoagiza mbele ya kufa kwake. Alikuwa amewaapisha Waisraeli akisema: “Mungu atakapowafikia kuwatoa katika inchi hii, munapaswa kupeleka mifupa yangu kutoka hapa pamoja nanyi.”


Mifupa ya Yosefu ambayo Waisraeli walikuwa wameileta kutoka Misri waliizika kule Sekemu katika eneo ambalo Yakobo alikuwa amelinunua kutoka kwa wana wa Hamori, baba ya Sekemu, kwa bei ya vikoroti mia moja vya feza. Eneo lile nalo likakuwa mali yao wazao wa Yosefu.


Wakati wa kufa kwake ulipokaribia, Yakobo akamwita mwana wake Yosefu, akamwambia: “Sasa, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, weka mukono wako chini ya mapaja yangu, uniahidi kwamba utanitendea kwa wema na uaminifu. Usinizike huku Misri,


Katika siku ya mwisho ya mwaka wa mia ine na makumi tatu, siku ileile ndipo makabila yote ya Yawe yaliondoka katika inchi ya Misri.


Siku hiyohiyo Yawe aliwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri kwa makundi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ