Jamii za watu zikutumikie, na mataifa yainame mbele yako kwa heshima. Ukuwe mutawala wa wandugu zako, na wana wa mama yako wainame mbele yako kwa heshima. Kila mutu anayekulaani alaaniwe, kila mutu anayekubariki abarikiwe!”
Mufalme akamupandisha katika gari lake la pili na walinzi wakatangulia mbele ya Yosefu wakilalamika kwa sauti na kusema: “Mupige magoti!” Ndivyo mufalme alivyomupa Yosefu madaraka makubwa juu ya inchi yote ya Misri.
Wakati ule Yosefu alikuwa mukubwa kule Misri. Yeye ndiye aliyekuwa akiwauzishia wanainchi ngano. Basi, kaka zake wakakuja na kuinama mbele ya Yosefu kwa heshima.
Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi ni Yosefu. Baba yangu angali muzima?” Lakini wandugu zake wakapigwa na bumbuazi mbele yake, hata wakashindwa kumujibu.
‘Mumwambie Yosefu kwa ajili yangu: Tafazali uwasamehe wandugu zako makosa yao mabaya na maovu yote waliyokutendea.’ Sasa basi, tafazali usamehe uovu tuliokutendea sisi watumishi wa Mungu wa baba yako.” Yosefu alipopata ujumbe huu, akalia.