Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 50:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 ‘Mumwambie Yosefu kwa ajili yangu: Tafazali uwasamehe wandugu zako makosa yao mabaya na maovu yote waliyokutendea.’ Sasa basi, tafazali usamehe uovu tuliokutendea sisi watumishi wa Mungu wa baba yako.” Yosefu alipopata ujumbe huu, akalia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 50:17
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kama Mungu wa babu yangu Abrahamu, Mungu ambaye ni kitisho cha Isaka, asingelikuwa upande wangu, hakika ungeliniacha niondoke mikono mitupu. Lakini Mungu aliona mateso yangu na kazi niliyofanya kwa mikono yangu, akakukaripia usiku wa kuamukia leo.”


Kwa hiyo, si ninyi mulionileta huku, lakini ni Mungu. Ndiye aliyenifanya kama baba kwa mufalme wa Misri, musimamizi wa nyumba yake yote na mutawala wa inchi yote ya Misri.


Mungu wa baba yako atakusaidia, Mungu Mwenye Nguvu atakubariki, upate baraka za mvua toka juu mbinguni, baraka za maji ya vilindi vinavyokuwa chini, baraka za uzazi wa wamama na nyama.


Kwa hiyo wakamupelekea Yosefu ujumbe, wakisema: “Baba yako, mbele hajakufa, aliagiza hivi:


Kisha wandugu zake wakamufikia, wakainama mpaka chini mbele yake, wakasema: “Sisi ni watumishi wako.”


Ninyi mulitaka kunitendea vibaya, lakini Mungu alikusudia mema kusudi watu wengi wapate kuwa wazima kama vile munavyoona leo.


Utawaangamiza wazao wao watoweke katika dunia; watoto wao hawatabaki kati ya wanadamu.


Anayeficha makosa yake hatafanikiwa, lakini anayeungama na kuyaacha atahurumiwa.


Na yeyote atakayetoa hata kikombe kimoja tu cha maji ya baridi kwa mumoja wa hao wanaokuwa wadogo kati ya wanafunzi wangu, kwa sababu yeye ni mwanafunzi wangu, kweli ninawaambia: mutu yule hatakosa kupewa zawadi yake.”


Yesu akaongeza kusema: “Ni hivi vilevile Baba yangu anayekuwa mbinguni atakavyowatendea ninyi, kama kila mumoja wenu asipomusamehe ndugu yake kwa moyo wake wote.”


Mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokitendea mumoja wa hawa wandugu zangu wanaohesabiwa kuwa wadogo, mulinitendea mimi.’


Utusamehe makosa yetu, kama sisi tunavyowasamehe wanaotukosea,


Wanafunzi wengine kumi waliposikia maneno yale, wakachukizwa na Yakobo na Yoane.


Basi, tunapokuwa bado na wakati, tufanye mema kwa watu wote, na zaidi kwa wandugu zetu katika imani.


Na wote wanaofuata kanuni hii katika maisha yao pamoja na watu wa Mungu wanaohesabiwa kama Waisraeli wa kweli, ninawatakia amani na wema.


Lakini mutendeane wema ninyi kwa ninyi; musameheane kama Mungu alivyowasamehe ninyi kwa njia ya Kristo.


Basi muitikiane zambi ninyi kwa ninyi na kuombeana kusudi mupate kuponyeshwa. Maombi ya bidii ya mwenye haki ni yenye faida kubwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ