Wakanana wenyeji wa inchi hiyo, walipoona maombolezo yaliyofanyika kwenye uwanja wa kupepetea ngano wa Atadi, wakasema: “Maombolezo haya ya Wamisri, kweli ni makubwa!” Kwa hiyo, pahali pale pakaitwa Abeli-Misri, napo pako ngambo ya muto Yordani.
wakamupeleka mpaka inchi ya Kanana, wakamuzika katika pango lililokuwa katika shamba kule Makipela, upande wa mashariki wa Mamure. Pango pamoja na shamba lile Abrahamu alikuwa amelinunua kwa Efuroni Muhiti, kusudi pakuwe pahali pake pa kuzikia.